1. Ninaapa kwa farasi wa Jihadi wendao mbio, na huku pumzi zao
zinasikilizana kwa sauti inayo itwa "Dh'abh'an".
2. Na kwa farasi hao ambao hutoa cheche za moto zinapo gonga
kwato zao kwenye ardhi wanapo kwenda.
3. Na kwa farasi hao wanao washambulia maadui asubuhi kabla jua
halijachomoza;
4. Wakatimua mavumbia mengi, farasi hao, kati ya makundi ya
maadui!
5. Ikawa vumbi limewagubika maadui hata wakaingiwa kiwewe na
kufazaika.
6. Hakika mwanaadamu ni mwingi wa kuzikufuru neema za Mola wake
Mlezi ambazo hazikadiriki.
7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka atakuwa mwingi wa kuja
jishuhudia huko Akhera kwa kuungama madhambi yake.
8. Na hakika yeye kwa uchoyo na kuyapenda mali alio nayo, ni
bakhili, hatoi kama inavyo mwajibikia katika mali yake.
9,10. Kwani hajui mwisho wa hali yake, hata hajui
wakitolewa maiti waliomo makaburini, na vikakusanywa viliomo vifuani navyo
vimekwisha sajiliwa katika madaftari yao, yakiwa mema au mabaya waliyo yatenda?
11. Kwamba hakika Mlezi wao na Muumba wao bila ya shaka anajua vyema vitendo vyao na malipo yao Siku ya Kufufuliwa na Kulipwa.