1. Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika usiku wa Cheo na
Utukufu.
2. Na kitu gani kitakufunza ni nini usiku huo wa Cheo na
Utukufu?
3. Usiku wa Qadr na Sharaf, Cheo na Utukufu, ni bora
kuliko miezi elfu, kwa kuwa umekhusika kwa kuteremka ndani yake Qur'ani tukufu.
4. Huteremka Malaika na Jibrili katika usiku huo mpaka kwenye
ardhi kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa sababu ya kila jambo.
5. Na wameaminika na maudhi na uovu. Hali inabaki hivyo mpaka mapambazuko ya alfajiri.