1. Ewe Muhammad! Soma unayo funuliwa kwa kufunguliwa kwa Jina
la Mola wako Mlezi ambaye ni Yeye tu peke yake ndiye Mwenye uweza wa kuumba.
2. Amemuumba mtu kwa ukamilifu wa mwili wake na ilimu kutokana
na kipande cha damu ambacho hakina chochote cha kupelekea kujiona bora.
3. Endelea na kusoma, na Mola wako Mlezi aliye Karimu kushinda
wote, atakutukuza wala hatakudharau.
4. Yeye ndiye ambaye aliye mfunza mtu kuandika kwa kalamu, na
wala kwanza hakuwa anajua hayo.
5. Amemfunza mtu yasiyo kuwa yanampitia katika mawazo yake.
6,7. Ni hakika kweli mtu hupindukia mpaka na hupanda
kiburi mbele ya Mola wake Mlezi anapo jiona si mhitaji, katajirika.
8. Ewe Muhammad! Hakika ni kwa Mola wako Mlezi peke yake ndiyo
yako marejeo ya wote kwa kufufuliwa na kulipwa.
9,10. Je! Umemwona huyu jeuri anaye mzuia mja
asisali anapo taka kusali?
11,12. Hebu niambie khabari za jeuri huyu kama yeye
yumo katika uwongofu katika huku kuzuia kwake, au kwamba ndio anaamrisha
uchamngu katika hayo anayo amrisha!
13. Niambie khabari za huyu mwenye kukataza anapo yakadhibisha
aliyo kuja nayo Mtume, na akapuuza Imani na vitendo vyema!
14. Hivyo hajui kwamba Mwenyezi Mungu anazijua vyema hali
zake, naye atamlipa kwazo?
15. Kwa kumkemea huyu mwenye kuzuia, anaambiwa kama hakuacha
hayo anayo yafanya, basi hapana shaka tutamkokota kwa nguvu tukimshika kwa
shungi lake la nywele mpaka Motoni!
16. Hilo shungi lilio juu ya uso wake mwenye kuropokwa uwongo
na mwenye athari za ukosefu!
17. Basi yeye awaite wenziwe na watu wa baraza lake wawe ndio
wasaidizi duniani au Akhera.
18. Sisi tutawaita askari wetu wamsaidie Muhammad na walio
pamoja naye, na wapambane na huyo mwenye kukanya na wasaidizi wawasukume kwenye
Jahannamu!
19. Kumnyamazisha huyu mwenye kuzuia, wewe usimkubalie kwa hayo anayo kukataza nayo, na dumu juu ya Sala zako, na endelea na sijida zako, na jijongeze kwa Mola wako Mlezi kwa hivyo.