1. Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;
2. Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na
cheo chake.
3. Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio
jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.
4. Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu
mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.
5. Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana
awezae kumdhalilisha?
6. Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na
kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.
7. Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui
yeyote hata huyo aliye muumba?
8,9. Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya
kutazamia, na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?
10. Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na
tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?
11. Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala
hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi
yake.
12. Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya
milimani?
13. Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,
15. Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.
16. Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.
17. Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao
usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.
18. Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa
mkono wa kulia.
19. Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha
Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa
kheri na watapata adhabu.
20. Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.