1,2,3. Kitakapo tukia Kiyama haitatokea nafsi yoyote ya kukadhibisha kutukia kwake. Kiyama hicho kitawateremsha chini walio waovu, na kitawanyanyua juu walio wema.
 

1,2,3. Kitakapo tukia Kiyama haitatokea nafsi yoyote ya kukadhibisha kutukia kwake. Kiyama hicho kitawateremsha chini walio waovu, na kitawanyanyua juu walio wema.
 

1,2,3. Kitakapo tukia Kiyama haitatokea nafsi yoyote ya kukadhibisha kutukia kwake. Kiyama hicho kitawateremsha chini walio waovu, na kitawanyanyua juu walio wema.
 

4,5,6. Ardhi itakapo tikiswa, na ikatetemeshwa kwa nguvu, na milima ikavurugwa teketeke, ikawa vumbi la kupeperushwa, Aya hizi tukufu zinaeleza hadi gani vitakuwa vitisho vitavyo uteremkia ulimwengu kitapo fika Kiyama. Na katika vitisho hivyo ni hayo masaibu ya dunia yatakayo athiri ardhi na mat'abaka yake. Kwani hii ardhi tunayo ishi juu ya mgongo wake si yenye kutulia na kukaa sawa kwa utimilivu. Kwani hiyo imeundwa kwa mat'abaka ya majabali yaliyo ingiliana ovyo. Huenda baadhi yao yakateremka yakaachana na mengineyo yaliyo jirani nayo. Na huwa hiyo inayo itwa kupasuka kwa mat'abaka ya ardhi, Geological cleavage kama inavyo tokea katika maeneo kadhaa wa kadhaa. Mpasuko huu ulikuwa na ungali kuwa ndio asili ya chini kabisa ya zilzala, mitetemeko, mikubwa kwa kuathirika na nguvu za kudidimiza na kuvuta zinazo fuatana na mat'abaka ya ardhi yanapo vunjika. Basi mizani ya utulivu ya nguvu hizi inapo geuka kwa kuathirika na mambo mengineyo ya nje huenda zikafunguka nguvu za mtikiso mkubwa ndio ikatokea mitetemeko na mitikisiko ya ardhi, ambayo hubomoa kila kitu kiliopo juu ya ardhi karibu na ilipo anzia hiyo zilzala. Na hapo tena hutokea uharibifu mkubwa mno. Na hayo maelezo ya kisayansi hayageuzi kitu, wala hayako mbali na nadhari ya kidini. Kwani hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu huenda akajaalia sababu za maumbile za kawaida zikajumuika kwa njia tusiyo izoea sisi ili zikiingiliana kwa njia ya kutisha ndio sababu ya kuharibika dunia. Hapo maelezo ya kisayansi yanafuatana na Aya zenye kuonya kwa vitisho hivyo vikuu. Na yote hayo yanatokana kwa Mwenyezi Mungu. Na hutokea kwa idhini yake Mwenyezi Mungu kutimiza hukumu yake katika dunia yetu
 

4,5,6. Ardhi itakapo tikiswa, na ikatetemeshwa kwa nguvu, na milima ikavurugwa teketeke, ikawa vumbi la kupeperushwa, Aya hizi tukufu zinaeleza hadi gani vitakuwa vitisho vitavyo uteremkia ulimwengu kitapo fika Kiyama. Na katika vitisho hivyo ni hayo masaibu ya dunia yatakayo athiri ardhi na mat'abaka yake. Kwani hii ardhi tunayo ishi juu ya mgongo wake si yenye kutulia na kukaa sawa kwa utimilivu. Kwani hiyo imeundwa kwa mat'abaka ya majabali yaliyo ingiliana ovyo. Huenda baadhi yao yakateremka yakaachana na mengineyo yaliyo jirani nayo. Na huwa hiyo inayo itwa kupasuka kwa mat'abaka ya ardhi, Geological cleavage kama inavyo tokea katika maeneo kadhaa wa kadhaa. Mpasuko huu ulikuwa na ungali kuwa ndio asili ya chini kabisa ya zilzala, mitetemeko, mikubwa kwa kuathirika na nguvu za kudidimiza na kuvuta zinazo fuatana na mat'abaka ya ardhi yanapo vunjika. Basi mizani ya utulivu ya nguvu hizi inapo geuka kwa kuathirika na mambo mengineyo ya nje huenda zikafunguka nguvu za mtikiso mkubwa ndio ikatokea mitetemeko na mitikisiko ya ardhi, ambayo hubomoa kila kitu kiliopo juu ya ardhi karibu na ilipo anzia hiyo zilzala. Na hapo tena hutokea uharibifu mkubwa mno. Na hayo maelezo ya kisayansi hayageuzi kitu, wala hayako mbali na nadhari ya kidini. Kwani hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu huenda akajaalia sababu za maumbile za kawaida zikajumuika kwa njia tusiyo izoea sisi ili zikiingiliana kwa njia ya kutisha ndio sababu ya kuharibika dunia. Hapo maelezo ya kisayansi yanafuatana na Aya zenye kuonya kwa vitisho hivyo vikuu. Na yote hayo yanatokana kwa Mwenyezi Mungu. Na hutokea kwa idhini yake Mwenyezi Mungu kutimiza hukumu yake katika dunia yetu.
 

4,5,6. Ardhi itakapo tikiswa, na ikatetemeshwa kwa nguvu, na milima ikavurugwa teketeke, ikawa vumbi la kupeperushwa, Aya hizi tukufu zinaeleza hadi gani vitakuwa vitisho vitavyo uteremkia ulimwengu kitapo fika Kiyama. Na katika vitisho hivyo ni hayo masaibu ya dunia yatakayo athiri ardhi na mat'abaka yake. Kwani hii ardhi tunayo ishi juu ya mgongo wake si yenye kutulia na kukaa sawa kwa utimilivu. Kwani hiyo imeundwa kwa mat'abaka ya majabali yaliyo ingiliana ovyo. Huenda baadhi yao yakateremka yakaachana na mengineyo yaliyo jirani nayo. Na huwa hiyo inayo itwa kupasuka kwa mat'abaka ya ardhi, Geological cleavage kama inavyo tokea katika maeneo kadhaa wa kadhaa. Mpasuko huu ulikuwa na ungali kuwa ndio asili ya chini kabisa ya zilzala, mitetemeko, mikubwa kwa kuathirika na nguvu za kudidimiza na kuvuta zinazo fuatana na mat'abaka ya ardhi yanapo vunjika. Basi mizani ya utulivu ya nguvu hizi inapo geuka kwa kuathirika na mambo mengineyo ya nje huenda zikafunguka nguvu za mtikiso mkubwa ndio ikatokea mitetemeko na mitikisiko ya ardhi, ambayo hubomoa kila kitu kiliopo juu ya ardhi karibu na ilipo anzia hiyo zilzala. Na hapo tena hutokea uharibifu mkubwa mno. Na hayo maelezo ya kisayansi hayageuzi kitu, wala hayako mbali na nadhari ya kidini. Kwani hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu huenda akajaalia sababu za maumbile za kawaida zikajumuika kwa njia tusiyo izoea sisi ili zikiingiliana kwa njia ya kutisha ndio sababu ya kuharibika dunia. Hapo maelezo ya kisayansi yanafuatana na Aya zenye kuonya kwa vitisho hivyo vikuu. Na yote hayo yanatokana kwa Mwenyezi Mungu. Na hutokea kwa idhini yake Mwenyezi Mungu kutimiza hukumu yake katika dunia yetu.
 

7. Na mkawa nyote siku hiyo namna tatu kwa mujibu wa vitendo vyenu;
 

8,9. Basi watu wa mkono wa kulia, watu wa cheo kilio bora, utukufu ulioje huo wa hali yao! Na watu wa kushotoni, hao ni watu wa cheo duni, uovu ulioje wa hali yao!
 

8,9. Basi watu wa mkono wa kulia, watu wa cheo kilio bora, utukufu ulioje huo wa hali yao! Na watu wa kushotoni, hao ni watu wa cheo duni, uovu ulioje wa hali yao!
 

10,11,12. Na walio tangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya Akhera. Hao ndio walio karibishwa mbele kwa Mwenyezi Mungu. Mola wao Mlezi atawatia katika Bustani zenye neema.
 

10,11,12. Na walio tangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya Akhera. Hao ndio walio karibishwa mbele kwa Mwenyezi Mungu. Mola wao Mlezi atawatia katika Bustani zenye neema.
 

10,11,12. Na walio tangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya Akhera. Hao ndio walio karibishwa mbele kwa Mwenyezi Mungu. Mola wao Mlezi atawatia katika Bustani zenye neema.
 

13,14. Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yaliyo tangulia na Manabii wao, na wachache katika umma wa Muhammad ukiwalinganisha na hao.
 

13,14. Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yaliyo tangulia na Manabii wao, na wachache katika umma wa Muhammad ukiwalinganisha na hao.
 

15,16. Juu ya viti au vitanda vilivyo nakishiwa kwa nakshi za vito vya thamani, wakivitegemea kwa raha na utulivu huku wakielekezana nyuso kwa ziada ya mahaba.
 

15,16. Juu ya viti au vitanda vilivyo nakishiwa kwa nakshi za vito vya thamani, wakivitegemea kwa raha na utulivu huku wakielekezana nyuso kwa ziada ya mahaba.
 

17,18. Wakiwazungukia kwa kuwakhudumia vijana watakao baki milele hivyo hivyo, nao wamechukua vikombe na mabirika yaliyo jaa vinywaji vya Peponi, na bilauri zenye mvinyo kutoka chemchem zinazo miminika,
 

17,18. Wakiwazungukia kwa kuwakhudumia vijana watakao baki milele hivyo hivyo, nao wamechukua vikombe na mabirika yaliyo jaa vinywaji vya Peponi, na bilauri zenye mvinyo kutoka chemchem zinazo miminika,
 

19. Vinywaji hivyo haviwaletei kuumwa kichwa wala kutokwa akili kwa ulevi.
 

20,21. Na matunda ya kila namna wanayo yapenda na wanayo yaona; na nyama za ndege kama zinavyo tamani nafsi zao.
 

20,21. Na matunda ya kila namna wanayo yapenda na wanayo yaona; na nyama za ndege kama zinavyo tamani nafsi zao.
 

22,23,24. Na wanawake wenye macho ya vikombe, kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa katika chaza, kwa usafi wao na urembo wao. Watapewa haya kuwa ni malipo kwa mambo mema waliyo kuwa wakiyatenda duniani.
 

22,23,24. Na wanawake wenye macho ya vikombe, kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa katika chaza, kwa usafi wao na urembo wao. Watapewa haya kuwa ni malipo kwa mambo mema waliyo kuwa wakiyatenda duniani.
 

22,23,24. Na wanawake wenye macho ya vikombe, kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa katika chaza, kwa usafi wao na urembo wao. Watapewa haya kuwa ni malipo kwa mambo mema waliyo kuwa wakiyatenda duniani.
 

25,26. Huko Peponi hawatasikia maneno yasiyo kuwa na maana, wala masimulizi ya kumtia dhambini mwenye kuyasikia. Ila watalo sikia ni kauli ya wao kwa wao: Tunakusalimuni kwa Salama.
 

25,26. Huko Peponi hawatasikia maneno yasiyo kuwa na maana, wala masimulizi ya kumtia dhambini mwenye kuyasikia. Ila watalo sikia ni kauli ya wao kwa wao: Tunakusalimuni kwa Salama.
 

27. Na watu wa mkono wa kulia, hapana ajuaye nini malipo ya watu wa kuliani.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

28,29,30,31,32,33,34. Katika miti ya mikunazi iliyo katwa miba yake, na migomba iliyo pangika na ndizi zake zimepandana juu ya mikungu, na kivuli kilicho enea wala hakiondoki, na maji yanayo miminika karibu yao popote wayatakapo, na matunda ya namna nyingi na kabila nyingi yasiyo tindikia wakati wowote, wala hazuiwiliwi ayatakayo, na matandiko yaliyo nyanyuliwa ya starehe.
 

35,36,37,38. Hakika Sisi tulianza kuwaumba Mahurulaini mwanzo, na tukawafanya kuwa ni vijana, wenye kupendwa na waume zao, wenye umri ulio karibiana, wa tayari kwa neema ya watu wa kuliani.
 

35,36,37,38. Hakika Sisi tulianza kuwaumba Mahurulaini mwanzo, na tukawafanya kuwa ni vijana, wenye kupendwa na waume zao, wenye umri ulio karibiana, wa tayari kwa neema ya watu wa kuliani.
 

35,36,37,38. Hakika Sisi tulianza kuwaumba Mahurulaini mwanzo, na tukawafanya kuwa ni vijana, wenye kupendwa na waume zao, wenye umri ulio karibiana, wa tayari kwa neema ya watu wa kuliani.
 

35,36,37,38. Hakika Sisi tulianza kuwaumba Mahurulaini mwanzo, na tukawafanya kuwa ni vijana, wenye kupendwa na waume zao, wenye umri ulio karibiana, wa tayari kwa neema ya watu wa kuliani.
 

39,40. Watu wa kulia ni wengi katika mataifu yaliyo kwisha tangulia, na kikundi kikubwa katika umma wa Muhammad.
 

39,40. Watu wa kulia ni wengi katika mataifu yaliyo kwisha tangulia, na kikundi kikubwa katika umma wa Muhammad.
 

41. Na watu wa kushoto, hapana anaye jua nini adhabu ya watu wa kushoto.
 

42,43,44. Watakuwa kwenye upepo umoto utakao wazunguka, unao penya katika tundu za mwili, na maji yaliyo chemshwa motoni wayanywe na wamiminiwe vichwani, na katika kivuli cha kiza cheusi cha moshi umoto, hapana ubaridi wa kupunguza joto la hewa, wala huruma ya kuwaletea nafuu wanapo vuta pumzi.
 

42,43,44. Watakuwa kwenye upepo umoto utakao wazunguka, unao penya katika tundu za mwili, na maji yaliyo chemshwa motoni wayanywe na wamiminiwe vichwani, na katika kivuli cha kiza cheusi cha moshi umoto, hapana ubaridi wa kupunguza joto la hewa, wala huruma ya kuwaletea nafuu wanapo vuta pumzi.
 

42,43,44. Watakuwa kwenye upepo umoto utakao wazunguka, unao penya katika tundu za mwili, na maji yaliyo chemshwa motoni wayanywe na wamiminiwe vichwani, na katika kivuli cha kiza cheusi cha moshi umoto, hapana ubaridi wa kupunguza joto la hewa, wala huruma ya kuwaletea nafuu wanapo vuta pumzi.
 

45. Hakika hao kabla ya haya walikuwa wamepita kiasi katika kustarehea neema za duniani, wamepumbaa hawataki kumt'ii Mwenyezi Mungu Mtukufu.
 

46. Na walikuwa wameshikilia daima kufanya dhambi kubwa kabisa, kwani waliapa kwa Mwenyezi Mungu kwamba kabisa Mwenyezi Mungu hatamfufua aliye kufa.
 

47. Na walikuwa wakisema kwa kukanusha kurejea tena: Ati tutafufuliwa baada ya kwisha kufa, na baadhi ya miili yetu ikisha kuwa udongo na mengine mifupa iliyo chakaa? Ati sisi tutarudishwa tuwe hai mara ya pili?
 

48. Ati tutafufuliwa sisi na baba zetu wa zamani walio kwisha kuwa udongo ulio tapanyika na umepotea katika ardhi?
 

49,50. Waambie kwa kuwajibu kukanusha kwao: Hakika wa zamani na wa mwisho, ambao nyinyi ni katika jumla ya hao, nyote mtakusanywa katika wakati wa siku malumu, na wala hamtoipita.
 

49,50. Waambie kwa kuwajibu kukanusha kwao: Hakika wa zamani na wa mwisho, ambao nyinyi ni katika jumla ya hao, nyote mtakusanywa katika wakati wa siku malumu, na wala hamtoipita.
 

51,52,53. Kisha nyinyi, enyi mnao ipinga Njia ya Uwongofu, mnao kanusha kufufuliwa, bila ya shaka mtakula mti wa Zaqqumu katika Jahannamu, na mtayajaza matumbo yenu kwa shida ya njaa.
 

51,52,53. Kisha nyinyi, enyi mnao ipinga Njia ya Uwongofu, mnao kanusha kufufuliwa, bila ya shaka mtakula mti wa Zaqqumu katika Jahannamu, na mtayajaza matumbo yenu kwa shida ya njaa.
 

51,52,53. Kisha nyinyi, enyi mnao ipinga Njia ya Uwongofu, mnao kanusha kufufuliwa, bila ya shaka mtakula mti wa Zaqqumu katika Jahannamu, na mtayajaza matumbo yenu kwa shida ya njaa.
 

54,55. Mtakunywa juu ya mlicho kila maji yenye kutokota, yasiyo ondoa kiu, na mtakunywa kwa wingi na pupa kama anavyo kunywa ngamia mwenye kiu kisicho katika kiu chake kwa maji.
 

54,55. Mtakunywa juu ya mlicho kila maji yenye kutokota, yasiyo ondoa kiu, na mtakunywa kwa wingi na pupa kama anavyo kunywa ngamia mwenye kiu kisicho katika kiu chake kwa maji.
 

56. Hayo yaliyo tajwa ya mateso mbali mbali ndio karamu yao waliyo andaliwa kwa siku ya malipo.
 

57. Sisi tulianza kukuumbeni mlipo kuwa si chochote, basi hebu hamkiri uweza wetu wa kukurejesheni tena baada ya kukufufueni?
 

58,59. Hamuangalii manii mnayo itia katika tumbo la uzazi? Ni nyinyi ndio mwenye uweza juu yake na kuilea mpaka ikawa mtu, au ni Sisi ndio twenye makadara hayo?
 

58,59. Hamuangalii manii mnayo itia katika tumbo la uzazi? Ni nyinyi ndio mwenye uweza juu yake na kuilea mpaka ikawa mtu, au ni Sisi ndio twenye makadara hayo?
 

60,61. Sisi tumekuhukumieni mauti, na tumeweka wakati makhsuri wa kufa kwenu. Na wala Sisi si wenye kushindwa kukubadilisheni sura zenu, na kuzileta nyengine, na tukakuumbeni katika umbo jengine na sura nyengine msiyo ijua.
 

60,61. Sisi tumekuhukumieni mauti, na tumeweka wakati makhsuri wa kufa kwenu. Na wala Sisi si wenye kushindwa kukubadilisheni sura zenu, na kuzileta nyengine, na tukakuumbeni katika umbo jengine na sura nyengine msiyo ijua.
 

62. Bila ya shaka mmekwisha yakinika kuwa Mwenyezi Mungu alikuumbeni mara ya kwanza, basi je, hamkumbuki kwamba Mwenye kuweza hayo ni Mweza zaidi wa kufanya tena.
 

63,64. Je! Hamuangalii mbegu mnayo ipanda katika ardhi? Ni nyinyi mnao ifanya imee au ni Sisi peke yetu ndio tunaifanya imee?
 

63,64. Je! Hamuangalii mbegu mnayo ipanda katika ardhi? Ni nyinyi mnao ifanya imee au ni Sisi peke yetu ndio tunaifanya imee?
 

65,66,67. Tungeli taka tungeli ifanya mimea hiyo iwe mabua na mapepe yaliyo katika katika kabla haijapevuka, mkawa mkistaajabu tu kwa uovu ulio isibu, huku mkisema: Hakika sisi tumepata khasara baada ya juhudi yetu. Bali sisi hatuna bahati, tumenyimwa riziki.
 

65,66,67. Tungeli taka tungeli ifanya mimea hiyo iwe mabua na mapepe yaliyo katika katika kabla haijapevuka, mkawa mkistaajabu tu kwa uovu ulio isibu, huku mkisema: Hakika sisi tumepata khasara baada ya juhudi yetu. Bali sisi hatuna bahati, tumenyimwa riziki.
 

65,66,67. Tungeli taka tungeli ifanya mimea hiyo iwe mabua na mapepe yaliyo katika katika kabla haijapevuka, mkawa mkistaajabu tu kwa uovu ulio isibu, huku mkisema: Hakika sisi tumepata khasara baada ya juhudi yetu. Bali sisi hatuna bahati, tumenyimwa riziki.
 

68,69. Je! Hamyaoni maji matamu mnayo yanywa? Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni, au ni Sisi ndio Wenye kuyateremsha kuwa ni rehema juu yenu? Katika Kiarabu limetajwa neno Almuzni. Maana yake ni mawingu yanayo leta mvua. Na kitendo cha kunyesha mvua kinahitajia mambo yaliyo khusiana na hali ya hewa maalumu ambayo mwanaadamu hana mamlaka nayo, au kuyaleta kwa juhudi zake. Kwa mfano zinahitajiwa pepo zinazo kwenda kwa mkondo zilizo baridi juu ya nyengine zilizo za joto, au hali za kuondoka utulivu katika anga. Na watu wamejaribu kuinyesha mvua kwa mawingu yanayo pita kwa njia ya ufundi, lakini juhudi hizo mpaka sasa ni majaribio, na lilio thibiti katika sayansi ni kufuzu kwa majaribio hayo ni kudogo mno, na hata hivyo kunalazimu ziwepo hali maalumu za maumbile zinazo saidia.
 

68,69. Je! Hamyaoni maji matamu mnayo yanywa? Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni, au ni Sisi ndio Wenye kuyateremsha kuwa ni rehema juu yenu? Katika Kiarabu limetajwa neno Almuzni. Maana yake ni mawingu yanayo leta mvua. Na kitendo cha kunyesha mvua kinahitajia mambo yaliyo khusiana na hali ya hewa maalumu ambayo mwanaadamu hana mamlaka nayo, au kuyaleta kwa juhudi zake. Kwa mfano zinahitajiwa pepo zinazo kwenda kwa mkondo zilizo baridi juu ya nyengine zilizo za joto, au hali za kuondoka utulivu katika anga. Na watu wamejaribu kuinyesha mvua kwa mawingu yanayo pita kwa njia ya ufundi, lakini juhudi hizo mpaka sasa ni majaribio, na lilio thibiti katika sayansi ni kufuzu kwa majaribio hayo ni kudogo mno, na hata hivyo kunalazimu ziwepo hali maalumu za maumbile zinazo saidia.
 

70. Lau tungeli taka tungeli yafanya hayo maji yakawa ya chumvi yasiyo nyweka. Basi mbona hamumshukuru Mwenyezi Mungu aliye yajaalia matamu yenye kunyweka?
 

71,72. Je! Hamuuoni moto huo mnao uasha? Ni nyinyi ndio mlio uotesha mti wake, na mkautia ndani ya huo mti moto, au ni Sisi ndio tulio uumbia hivyo, kadhaalika?
 

71,72. Je! Hamuuoni moto huo mnao uasha? Ni nyinyi ndio mlio uotesha mti wake, na mkautia ndani ya huo mti moto, au ni Sisi ndio tulio uumbia hivyo, kadhaalika?
 

73. Sisi tumeufanya huu moto uwe ni ukumbusho wa Moto wa Jahannamu mtapo uona, na uwe ni manufaa kwa wasafiri wa msitu na nyika, wakinafiika kwa kupikia chakula chao na kuotea moto wakati wa baridi.
 

74. Basi dumisha kusabihi, kutakasa, kwa kulidhukuru jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa, kwa kumtakasa na kumshukuru kwa neema hizi nzuri.
 

75,76. Basi ninaapa kweli kwa maangukio ya nyota pale zinapo tua mwisho wa usiku wakati wa Tahajudi, ibada za usiku, na kustaghafiru. Na hakika bila ya shaka hicho ni kiapo kikubwa chenye maana ya kufikia mbali, lau kuwa mnafikiri makusudio yake. Aya mbili hizi zinabainisha hadi ya umuhimu wa kiapo hichi kikubwa. Kwani nyota ni vitu vyenye kutoa mwangaza wenyewe, na nyota ya karibu mno kwetu sisi, nayo ni jua, ni kiasi ya masafa ya miaka 500 ya mwangaza. Na nyota ifuatayo kwa ukaribu iko mbali nasi kwa kiasi cha miaka 4 ya mwangaza takriban. Basi nguvu tunazo zitumia kutokana na jua ndizo zinazo tuwezesha kuishi. Lau kuwa umbali wa jua kutokana na ardhi ni duni ya hivyo au zaidi ya hivyo basi hapana shaka kuwa maisha yangeli kuwa taabu, bali ni muhali. Kadhaalika ukubwa wa nyota unakhitalifiana. Zipo nyota kubwa mno hata ukubwa wake unaweza kukusanya hii ardhi na jua juu ya umbali wao. Vipo vikundi vya nyota vinavyo itwa A'naqiid vinaogelea angani zikivuka Njia ya Maziwa The Milky Way mara kwa mara. Wakati wa kupita kwake zikasadifiana kukutana na kikundi cha jua na zikagongana basi hakika hapo itakuwa ndio maangamizo na kumalizika kwa kweli. Hata ikikaribia nyota moja katika nyota zitokazo kwenye jua basi hayo pia yataleta kuharibika mizani na kupelekea maangamizo na kumalizika ulimwengu. Kwa hivyo basi hakika Ishara za mazingatio na uweza wa Mwenyezi Mungu zinaonekana katika ulimwengu huu alio uumba Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala na akaupanga.
 

75,76. Basi ninaapa kweli kwa maangukio ya nyota pale zinapo tua mwisho wa usiku wakati wa Tahajudi, ibada za usiku, na kustaghafiru. Na hakika bila ya shaka hicho ni kiapo kikubwa chenye maana ya kufikia mbali, lau kuwa mnafikiri makusudio yake. Aya mbili hizi zinabainisha hadi ya umuhimu wa kiapo hichi kikubwa. Kwani nyota ni vitu vyenye kutoa mwangaza wenyewe, na nyota ya karibu mno kwetu sisi, nayo ni jua, ni kiasi ya masafa ya miaka 500 ya mwangaza. Na nyota ifuatayo kwa ukaribu iko mbali nasi kwa kiasi cha miaka 4 ya mwangaza takriban. Basi nguvu tunazo zitumia kutokana na jua ndizo zinazo tuwezesha kuishi. Lau kuwa umbali wa jua kutokana na ardhi ni duni ya hivyo au zaidi ya hivyo basi hapana shaka kuwa maisha yangeli kuwa taabu, bali ni muhali. Kadhaalika ukubwa wa nyota unakhitalifiana. Zipo nyota kubwa mno hata ukubwa wake unaweza kukusanya hii ardhi na jua juu ya umbali wao. Vipo vikundi vya nyota vinavyo itwa A'naqiid vinaogelea angani zikivuka Njia ya Maziwa The Milky Way mara kwa mara. Wakati wa kupita kwake zikasadifiana kukutana na kikundi cha jua na zikagongana basi hakika hapo itakuwa ndio maangamizo na kumalizika kwa kweli. Hata ikikaribia nyota moja katika nyota zitokazo kwenye jua basi hayo pia yataleta kuharibika mizani na kupelekea maangamizo na kumalizika ulimwengu. Kwa hivyo basi hakika Ishara za mazingatio na uweza wa Mwenyezi Mungu zinaonekana katika ulimwengu huu alio uumba Mwenyezi Mungu Subhanahu wa Taala na akaupanga.
 

77,78. Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani yenye manufaa mengi, imo katika ubao ulio hifadhiwa Al-lauhu-lmahfudh, usio karibiwa na yeyote ila Malaika walio karibishwa kwa Mwenyezi Mungu. (Kwa watumiaji Computer wanaweza kukisia kuwa hiyo Al-lauhu-lmahfudh ni kama Disk iliyomo ndani ya Computer na haigusi mtu, na Misahafu tunayo iona, na kuisoma, ni kama yapigwayo chapa kutoka hiyo Disk.)
 

77,78. Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani yenye manufaa mengi, imo katika ubao ulio hifadhiwa Al-lauhu-lmahfudh, usio karibiwa na yeyote ila Malaika walio karibishwa kwa Mwenyezi Mungu. (Kwa watumiaji Computer wanaweza kukisia kuwa hiyo Al-lauhu-lmahfudh ni kama Disk iliyomo ndani ya Computer na haigusi mtu, na Misahafu tunayo iona, na kuisoma, ni kama yapigwayo chapa kutoka hiyo Disk.)
 

79,80. Hawaigusi Qur'ani Tukufu ila walio t'ahirika na najisi na hadathi, vitengua udhu; imeteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe vyote.
 

79,80. Hawaigusi Qur'ani Tukufu ila walio t'ahirika na najisi na hadathi, vitengua udhu; imeteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe vyote.
 

81. Je! Mnapuuza? Ni Qur'ani hii tukufu ndio nyinyi mnaidharau?
 

82. Na badala ya kuishukuru riziki yenu ndio mna ikadhibisha?
 

83,84,85. Basi je! Ikifika roho ya mmoja wenu kwenye mapitio ya pumzi, na nyinyi inapo fika roho kwenye koo nanyi mnamwangalia huyo anaye kufa, na Sisi tuko karibu zaidi kwa huyo aliye kabiliwa na mauti na tunaijua zaidi hali yake kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamjui hayo wala hamhisi.
 

83,84,85. Basi je! Ikifika roho ya mmoja wenu kwenye mapitio ya pumzi, na nyinyi inapo fika roho kwenye koo nanyi mnamwangalia huyo anaye kufa, na Sisi tuko karibu zaidi kwa huyo aliye kabiliwa na mauti na tunaijua zaidi hali yake kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamjui hayo wala hamhisi.
 

83,84,85. Basi je! Ikifika roho ya mmoja wenu kwenye mapitio ya pumzi, na nyinyi inapo fika roho kwenye koo nanyi mnamwangalia huyo anaye kufa, na Sisi tuko karibu zaidi kwa huyo aliye kabiliwa na mauti na tunaijua zaidi hali yake kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamjui hayo wala hamhisi.
 

86,87. Basi je! Ikiwa nyinyi si wenye kunyenyekea kwa Ungu wetu, mrudishieni roho yake huyo aliye kabiliwa na mauti ikiwa nyinyi mwasema kweli kwamba nyinyi mnazo nguvu na hamshindwi.
 

86,87. Basi je! Ikiwa nyinyi si wenye kunyenyekea kwa Ungu wetu, mrudishieni roho yake huyo aliye kabiliwa na mauti ikiwa nyinyi mwasema kweli kwamba nyinyi mnazo nguvu na hamshindwi.
 

88,89. Ama akiwa huyo aliye kabiliwa na mauti ni katika walio tangulia walio karibishwa basi mwisho wake ni raha, na rehema, na riziki njema, na Pepo yenye neema.
 

88,89. Ama akiwa huyo aliye kabiliwa na mauti ni katika walio tangulia walio karibishwa basi mwisho wake ni raha, na rehema, na riziki njema, na Pepo yenye neema.
 

90,91. Ama akiwa katika watu wa mkono wa kulia, basi ataambiwa kwa maamkio na takrima: Unapewa salamu kutokana na watu wa kuliani.
 

90,91. Ama akiwa katika watu wa mkono wa kulia, basi ataambiwa kwa maamkio na takrima: Unapewa salamu kutokana na watu wa kuliani.
 

92,93,94. Na ama akiwa ni katika wa kushoto, wanao kanusha, walio wapotovu, basi atakirimiwa maji ya moto hadi ya kuchemka, na kubabuliwa na moto wa mwisho wa ukali.
 

92,93,94. Na ama akiwa ni katika wa kushoto, wanao kanusha, walio wapotovu, basi atakirimiwa maji ya moto hadi ya kuchemka, na kubabuliwa na moto wa mwisho wa ukali.
 

92,93,94. Na ama akiwa ni katika wa kushoto, wanao kanusha, walio wapotovu, basi atakirimiwa maji ya moto hadi ya kuchemka, na kubabuliwa na moto wa mwisho wa ukali.
 

95. Hakika haya yaliyo tajwa katika Sura hii tukufu bila ya shaka ni kiini cha yakini iliyo thibiti, isiyo ingiliwa na shaka.
 

96. Tanguliza tasbihi kwa kumdhukuru Mola wako Mlezi aliye Mkubwa, kwa kumtakasa na kumshukuru kwa neema zake.
 

Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani