Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

43.Surat Az-Zukhruf


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. H'a Mim
1

image
2. Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
2

image
3. Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
3

image
4. Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
4

image
5. Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
5

image
6. Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
6

image
7. Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
7

image
8. Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
8

image
9. Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
9

image
10. Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
10

image
11. Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
11

image
12. Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
12

image
13. Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
13

image
14. Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
14

image
15. Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
15

image
16. Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
16

image
17. Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
17

image
18. Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
18

image
19. Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
19

image
20. Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
20

image
21. Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
21

image
22. Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
22

image
23. Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
23

image
24. Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
24

image
25. Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
25

image
26. Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
26

image
27. Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
27

image
28. Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
28

image
29. Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
29

image
30. Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
30

image
31. Na walisema: Kwa nini Qur'ani hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?
31

image
32. Kwani wao ndio wanao gawa rehema za Mola wako Mlezi? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawanyanyua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wenginewe wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayo yakusanya.
32

image
33. Na lau isinge kuwa watu watakuwa kundi moja tungeli wajaalia wanao mkufuru Rahmani wana nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazo pandia,
33

image
34. Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyo egemea juu yake,
34

image
35. Na mapambo. Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako Mlezi ni ya wenye kumchamngu.
35

image
36. Anaye yafanyia upofu maneno ya Rahmani tunamwekea Shet'ani kuwa ndiye rafiki yake.
36

image
37. Na hakika wao wanawazuilia Njia na wenyewe wanadhani kuwa wameongoka.
37

image
38. Hata atakapo tujia atasema: Laiti ungeli kuwako baina yangu na wewe kama umbali baina ya mashariki na magharibi. Rafiki mwovu mno wewe!
38

image
39. Na kwa kuwa mlidhulumu, haitakufaeni kitu leo kwamba nyinyi mnashirikiana katika adhabu.
39

image
40. Je! Unaweza kuwasikilizisha viziwi, au unaweza kuwaongoa vipofu na waliomo katika upotofu ulio wazi?
40

image
41. Na hata tukikuondoa, Sisi tutalipiza kisasi chetu kwao.
41

image
42. Au tutakuonyesha tulio waahidi. Nasi bila ya shaka tuna uweza juu yao.
42

image
43. Basi wewe yashike yaliyo funuliwa kwako. Hakika wewe uko kwenye Njia Iliyo Nyooka.
43

image
44. Na hakika haya ni ukumbusho kwako na kwa kaumu yako. Na mtakuja ulizwa.
44

image
45. Na waulize Mitume wetu tulio watuma kabla yako: Je! Tulifanya miungu mingine iabudiwe badala ya Rah'mani?
45

image
46. Na bila ya shaka tulimtuma Musa kwa Ishara zetu ende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!
46

image
47. Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaingia kuzicheka.
47

image
48. Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyenginewe. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee.
48

image
49. Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyo kuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka.
49

image
50. Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi.
50

image
51. Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamwoni?
51

image
52. Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?
52

image
53. Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?
53

image
54. Basi aliwachezea watu wake, na wakamt'ii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu.
54

image
55. Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
55

image
56. Walipo tukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!
56

image
57. Na alipo pigiwa mfano Mwana wa Mariamu, watu wako waliupiga ukelele.
57

image
58. Wakasema: Miungu yetu kwani si bora kuliko huyu? Hawakukupigia mfano huo ila kwa ubishi tu. Bali hao ni watu wagomvi!
58

image
59. Hakuwa yeye (Isa) ila ni Mtumwa tuliye mneemesha na tukamfanya ni mfano kwa Wana wa Israili.
59

image
60. Na tungeli penda tungeli wafanyia miongoni mwenu Malaika katika ardhi wakifuatana.
60

image
61. Na kwa hakika yeye ni alama ya Saa ya Kiyama. Basi usiitilie shaka, na nifuateni. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
61

image
62. Wala asikuzuilieni Shet'ani. Hakika yeye ni adui yenu wa dhaahiri.
62

image
63. Na alipo kuja Isa na dalili zilizo wazi, alisema: Nimekujieni na hikima, na ili nikuelezeni baadhi ya yale mliyo khitalifiana. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na mnit'ii mimi.
63

image
64. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mola wangu Mlezi, na ni Mola wenu Mlezi. Basi Muabuduni Yeye tu. Hii ndiyo Njia Iliyo Nyooka.
64

image
65. Lakini makundi kwa makundi yao yalikhitalifiana wao kwa wao. Ole wao walio dhulumu kwa adhabu ya siku chungu.
65

image
66. Je! Nini wanangojea ila Saa iwajie kwa ghafla na wala wao hawatambui?
66

image
67. Siku hiyo marafiki watakuwa ni maadui, wao kwa wao, isipo kuwa wachamngu.
67

image
68. Enyi waja wangu! Hamtakuwa na khofu siku hiyo, wala hamtahuzunika.
68

image
69. Ambao waliziamini Ishara zangu na walikuwa Waislamu.
69

image
70. Ingieni Peponi, nyinyi na wake zenu; mtafurahishwa humo.
70

image
71. Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele.
71

image
72. Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
72

image
73. Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala.
73

image
74. Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu.
74

image
75. Hawatapumzishwa nayo na humo watakata tamaa.
75

image
76. Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhaalimu.
76

image
77. Nao watapiga kelele waseme: Ewe Malik! Na atufishe Mola wako Mlezi! Naye aseme: Hakika nyinyi mtakaa humo humo!
77

image
78. Kwa yakini tulikuleteeni Haki, lakini wengi katika nyinyi mlikuwa mnaichukia Haki.
78

image
79. Au waliweza kupitisha amri yao? Bali ni Sisi ndio tunao pitisha.
79

image
80. Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong'ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika.
80

image
81. Sema: Ingeli kuwa Rahmani ana mwana, basi mimi ningeli kuwa wa kwanza kumuabudu.
81

image
82. Ametakasika Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, Mola Mlezi wa A'rshi, na hayo wanayo msifia.
82

image
83. Basi waache wapige porojo wakicheza mpaka wakutwe na hiyo siku yao waliyo ahidiwa.
83

image
84. Na Yeye ndiye Mungu mbinguni, na ndiye Mungu katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hikima, Mwenye ujuzi.
84

image
85. Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa.
85

image
86. Wala hao mnao waomba badala yake Yeye hawana uweza wa kumwombea mtu, isipo kuwa anaye shuhudia kwa haki, na wao wanajua.
86

image
87. Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu! Basi ni wapi wanako geuziwa?
87

image
88. Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini.
88

image
89. Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua.
89


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani