Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

52.Surat At-Tur


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa mlima wa T'ur,
1

image
2. Na Kitabu kilicho andikwa
2

image
3. Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
3

image
4. Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
4

image
5. Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
5

image
6. Na kwa bahari iliyo jazwa,
6

image
7. Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
7

image
8. Hapana wa kuizuia.
8

image
9. Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
9

image
10. Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
10

image
11. Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
11

image
12. Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
12

image
13. Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
13

image
14. (Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
14

image
15. Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
15

image
16. Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
16

image
17. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
17

image
18. Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
18

image
19. Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
19

image
20. Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
20

image
21. Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
21

image
22. Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
22

image
23. Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
23

image
24. Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
24

image
25. Wataelekeana wakiulizana.
25

image
26. Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
26

image
27. Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
27

image
28. Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
28

image
29. Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
29

image
30. Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
30

image
31. Sema: Tarajieni, na mimi pia ni pamoja nanyi katika kutarajia.
31

image
32. Au hizo akili zao ndio zinawaamrisha haya, au wao basi ni watu majeuri tu?
32

image
33. Au ndio wanasema: Ameitunga hii! Bali basi tu hawaamini!
33

image
34. Basi nawalete masimulizi kama haya ikiwa wao wanasema kweli.
34

image
35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?
35

image
36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.
36

image
37. Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?
37

image
38. Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi!
38

image
39. Au Yeye Mwenyezi Mungu ana wasichana, na nyinyi ndio mna wavulana?
39

image
40. Au wewe unawaomba ujira, na kwa hivyo ndio wanaelemewa na uzito wa gharama?
40

image
41. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wameandika?
41

image
42. Au wanataka kufanya vitimbi tu? Lakini hao walio kufuru ndio watakao tegeka.
42

image
43. Au wanae mungu asiye kuwa Mwenyezi Mungu? Subhanallah! Ametaksika Mwenyezi Mungu na hao wanao washirikisha naye.
43

image
44. Na hata wange ona pande linatoka mbinguni linaanguka wange sema: Ni mawingu yaliyo bebana.
44

image
45. Basi waache mpaka wakutane na siku yao watakapo hilikishwa.
45

image
46. Siku ambayo hila zao hazitawafaa hata kidogo, wala wao hawatanusuriwa.
46

image
47. Na hakika walio dhulumu watapata adhabu nyengine isiyo kuwa hii, lakini wengi wao hawajui.
47

image
48. Na ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi. Kwani wewe hakika uko mbele ya macho yetu, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi unapo simama,
48

image
49. Na usiku pia mtakase, na zinapo kuchwa nyota. 
49


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani