Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

95.Surat At-Tin


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa tini na zaituni!
1

image
2. Na kwa Mlima wa Sinai!
2

image
3. Na kwa mji huu wenye amani!
3

image
4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.
4

image
5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
5

image
6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.
6

image
7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
7

image
8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?
8


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani