Tarjuma ya Quran Tukufu
kwa kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU
MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

1. Naapa kwa tini na zaituni! 1

2. Na kwa Mlima wa Sinai! 2

3. Na kwa mji huu wenye amani! 3

4. Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora
kabisa. 4

5. Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
5

6. Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao
watapata ujira usio kwisha. 6

7. Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
7

8. Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu
wote? 8
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin
Al-Barwani
Ikiwa
una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com
Copyright � 22 August 1997, Sheikh
Ali Muhsin Al Barwani