Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

81.Surat At-Takwir


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Jua litakapo kunjwa,
1

image
2. Na nyota zikazimwa,
2

image
3. Na milima ikaondolewa,
3

image
4. Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
41

image
5. Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
5

image
6. Na bahari zikawaka moto,
6

image
7. Na nafsi zikaunganishwa,
7

image
8. Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
8

image
9. Kwa kosa gani aliuliwa?
9

image
10. Na madaftari yatakapo enezwa,
10

image
11 Na mbingu itapo tanduliwa,
11

image
12. Na Jahannamu itapo chochewa,
12

image
13. Na Pepo ikasogezwa,
13

image
14. Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
14

image
15. Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
15

image
16. Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
16

image
17. Na kwa usiku unapo pungua,
17

image
18. Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
18

image
19. Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
19

image
20. Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
20

image
21. Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
21

image
22. Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
22

image
23. Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
23

image
24. Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
24

image
25. Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
25

image
26. Basi mnakwenda wapi?
26

image
27. Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
27

image
28. Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
28

image
29. Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
29


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani