Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

86.Surat At-Taariq


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
1

image
2. Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
2

image
3. Ni Nyota yenye mwanga mkali.
3

image
4. Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
4

image
5. Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
5

image
6. Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
6

image
7. Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
7

image
8. Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
8

image
9. Siku zitakapo dhihirishwa siri.
9

image
10. Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
10

image
11. Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
11

image
12 Na kwa ardhi inayo pasuka!
12

image
13. Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
13

image
14. Wala si mzaha.
14

image
15. Hakika wao wanapanga mpango.
15

image
16. Na Mimi napanga mpango.
16

image
17. Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.
17


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani