Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

91.Surat Ash-Shams


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa jua na mwangaza wake!
1

image
2. Na kwa mwezi unapo lifuatia!
2

image
3. Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
3

image
4. Na kwa usiku unapo lifunika!
4

image
5. Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
5

image
6. Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
6

image
7. Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
7

image
8. Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
8

image
9. Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
9

image
10. Na hakika amekhasiri aliye iviza.
10

image
11. Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
11

image
12. Alipo simama mwovu wao mkubwa,
12

image
13. Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
13

image
14. Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
14

image
15. Wala Yeye haogopi matokeo yake.
15


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani