Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

26.Surat As-Shu'araa


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. T'aa Siin Miim. (T'.S.M.)
1

image
2. Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
2

image
3. Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
3

image
4. Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
4

image
5. Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
5

image
6. Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
6

image
7. Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
7

image
8. Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
8

image
9. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
9

image
10. Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
10

image
11. Watu wa Firauni. Hawaogopi?
11

image
12. Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
12

image
13. Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
13

image
14. Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
14

image
15. Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
15

image
16. Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
16

image
17. Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
17

image
18. (Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
18

image
19. Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
19

image
20. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
20

image
21. (Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
21

image
22. Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
22

image
23. Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
23

image
24. Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
24

image
25. (Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
25

image
26. (Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
26

image
27. (Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
27

1 image
28. (Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
28

image
29. (Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
29

image
30. Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
30

image
31. Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli.
31

image
32. Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri.
32

image
33. Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao.
33

image
34. (Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
34

image
35. Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
35

image
36. Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo.
36

image
37. Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
37

image
38. Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu.
38

image
39. Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?
39

image
40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda.
40

image
41. Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?
41

image
42. Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
42

image
43. Musa akwaambia: Tupeni mnavyo taka kutupa.
43

image
44. Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
44

image
45. Musa tena akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza walivyo vizua.
45

image
46. Hapo wachawi walipinduka wakasujudu.
46

image
47. Wakasema: Tunamuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
47

image
48. Mola Mlezi wa Musa na Harun.
48

image
49. (Firauni) akasema: Je! Mmemuamini kabla sijakuruhusuni? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliye kufunzeni uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakubandikeni misalabani nyote.
49

image
50. Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
50

image
51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa ndio wa kwanza wa kuamini.
51

image
52. Na tulimuamrisha Musa kwa wahyi: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
52

image
53. Basi Firauni akawatuma mijini wapiga mbiu za mgambo.
53

image
54. (Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
54

image
55. Nao wanatuudhi.
55

image
56. Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
56

image
57. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem,
57

image
58. Na makhazina, na vyeo vya hishima,
58

image
59. Kadhaalika; na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
59

image
60. Basi wakawafuata lilipo chomoza jua.
60

image
61. Na yalipo onana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!
61

image
62. (Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
62

image
63. Tulimletea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
63

image
64. Na tukawajongeza hapo wale wengine.
64

image
65. Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote.
65

image
66. Kisha tukawazamisha hao wengine.
66

image
67. Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini.
67

image
68. Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
68

image
69. Na wasomee khabari za Ibrahim.
69

image
70. Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
70

image
71. Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
71

image
72. Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?
72

image
73. Au yanakufaeni, au yanakudhuruni?
73

image
74. Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
74

image
75. Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-
75

image
76. Nyinyi na baba zenu wa zamani?
76

image
77. Kwani hakika hao ni adui zangu, isipo kuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
77

image
78. Ambaye ndiye aliye niumba, na Yeye ndiye ananiongoa,
78

image
79. Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
79

image
80. Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha.
80

image
81. Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
81

image
82. Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
82

image
83. Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema.
83

image
84. Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye.
84

image
85. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.
85

image
86. Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
86

image
87. Wala usinihizi Siku watapo fufuliwa.
87

image
88. Siku ambayo kwamba mali hayato faa kitu wala wana.
88

image
89. Isipo kuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
89

image
90. Na Pepo itasogezwa kwa wachamngu.
90

image
91. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
91

image
92. Na wataambiwa: Wako wapi mlio kuwa mkiwaabudu
92

image
93. Badala ya Mwenyezi Mungu? Je! Wanakusaidieni, au wanajisaidia wenyewe?
93

image
94. Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,
94

image
95. Na majeshi ya Ibilisi yote.
95

image
96. Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
96

image
97. Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhaahiri,
97

image
98. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
98

image
99. Tulipo kufanyeni ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
99

image
100. Basi hatuna waombezi.
100

image
101. Wala rafiki wa dhati.
101

image
102. Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.
102

image
103. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
103

image
104. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
104

image
105. Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
105

image
106. Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?
106

image
107. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
107

image
108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
108

image
109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
109

image
110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
110

image
111. Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?
111

image
112. Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?
112

image
126. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!
113

image
114. Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
114

image
115. Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.
115

image
116. Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
116

image
117. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.
117

image
118. Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.
118

image
119. Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.
119

image
120. Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.
120

image
121. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
121

image
122. Kina A'd waliwakanusha Mitume.
122

image
123. Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?
123

image
124. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
124

image
125. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
125

image
126. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
126

image
127. Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
127

image
128. Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!
128

image
129. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
129

image
130. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.
130

image
131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
131

image
132. Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.
132

image
133. Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.
133

image
134. Na mabustani na chemchem.
134

image
135. Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.
135

image
136. Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
136

image
137. Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
137

image
138. Wala sisi hatutaadhibiwa.
138

image
139. Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
139

image
140. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
140

image
141. Kina Thamud waliwakanusha Mitume.
141

image
142. Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?
142

image
143. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
143

image
144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.
144

image
145. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
145

image
146. Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
146

image
147. Katika mabustani, na chemchem?
147

image
148. Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.
148

image
149. Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
149

image
150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
150

image
151. Wala msit'ii amri za walio pindukia mipaka,
151

image
152. Ambao wanafanya ufisadi katika nchi, wala hawatengenezi.
152

image
153. Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa walio rogwa.
153

image
154. Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete Ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
154

image
155. Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
155

image
156. Wala msimguse kwa uwovu, isije ikakushikeni adhabu ya Siku Kubwa.
156

image
157. Lakini wakamuuwa, na wakawa wenye kujuta.
157

image
158. Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
158

image
159. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
159

image
160. Watu wa Lut'i waliwakanusha Mitume.
160

image
161. Alipo waambia ndugu yao, Lut'i: Je! Hamumchimngu?
161

image
162. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
162

image
163. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nit'iini mimi.
163

image
164. Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
164

image
165. Je! Katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
165

image
166. Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnao ruka mipaka!
166

image
167. Wakasema: Ewe Lut'i! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!
167

image
168. Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu.
168

image
169. Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
169

image
170. Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,
170

image
171. Isipo kuwa kikongwe katika walio kaa nyuma.
171

image
172. Kisha tukawaangamiza wale wengine.
172

image
173. Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyo onywa.
173

image
174. Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
174

image
175. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
175

image
176. Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
176

image
177. Shuaibu alipo waambia: Je! Hamfanyi mkamchamngu?
177

image
178. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
178

image
179. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.
179

image
180. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
180

image
181. Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja.
181

image
182. Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;
182

image
183. Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi.
183

image
184. Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia.
184

image
185. Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa.
185

image
186. Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
186

image
187. Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.
187

image
188. Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda.
188

image
189. Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.
189

image
190. Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
190

image
191. Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
191

image
192. Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
192

image
193. Ameuteremsha Roho muaminifu,
193

image
194. Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,
194

image
195. Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
195

image
196. Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
196

image
197. Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?
197

image
198. Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,
198

image
199. Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini.
1990

image
200. Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.
200

image
201. Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
201

image
202. Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari.
202

image
203. Na watasema: Je, tutapewa muhula?
203

image
204. Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?
204

image
205. Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka,
205

image
206. Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,
206

image
207. Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?
207

image
208. Wala hatukuangamiza mji wo wote ila ulikuwa na waonyaji
208

image
209. Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
209

image
210. Wala Mashet'ani hawakuteremka nayo,
10

image
211. Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
11

image
212. Hakika hao wametengwa na kusikia.
12

image
213. Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakao adhibiwa.
13

image
214. Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
14

image
215. Na watwae kwa upole wanao kufuata miongoni mwa Waumini.
15

image
216. Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi najitenga mbali na hayo mnayo yatenda.
16

image
217. Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
17

image
218. Ambaye anakuona unapo simama,
18

image
219. Na mageuko yako kati ya wanao sujudu.
19

image
220. Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua.
20

image
221. Je! Nikwambieni nani wanawashukia Mashet'ani?
21

image
222. Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
22

image
223. Wanawapelekea yale wanayo yasikia; na wengi wao ni waongo.
23

image
224. Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
24

image
225. Je! Huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
25

image
226. Na kwamba wao husema wasiyo yatenda?
26

image
227. Isipo kuwa wale walio amini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapo dhulumiwa. Na wanao dhulumu watakuja jua mgeuko gani watakao geuka.
27


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani