Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

Surat Ar-Rahmaan


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. Arrah'man, Mwingi wa Rehema
1

image
2. Amefundisha Qur'ani.
2

image
3. Amemuumba mwanaadamu,
3

image
4. Akamfundisha kubaini.
4

image
5. Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
5

image
6. Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
6

image
7. Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
7

image
8. Ili msidhulumu katika mizani.
8

image
9. Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
9

image
10. Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
10

image
11. Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
11

image
12. Na nafaka zenye makapi, na rehani.
12

image
13. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
13

image
14. Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo.
14

image
15. Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
15

image
16. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
16

image
17. Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
17

image
18. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
18

image
19. Anaziendesha bahari mbili zikutane;
19

image
20. Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
20

image
21. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
21

image
22. Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
22

image
23. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
23

image
24. Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
24

image
25. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
25

image
26. Kila kilioko juu yake kitatoweka.
26

image
27. Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
27

image
28. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
28

image
29. Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
29

image
30. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
30

image
31. Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.
31

image
32. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
32

image
33. Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.
33

image
34. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
34

image
35. Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.
35

image
36. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
36

image
37. Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.
37

image
38. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
38

image
39. Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.
39

image
40. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
40

image
41. Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.
41

image
42. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
42

image
43. Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.
43

image
44. Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.
44

image
45. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
45

image
46. Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.
46

image
47. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
47

image
48. Bustani zenye matawi yaliyo tanda.
48

image
49. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
49

image
50. Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.
50

image
51. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
51

image
52. Humo katika kila matunda zimo namna mbili.
52

image
53. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
53

image
54. Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.
54

image
55. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
55

image
56. Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.
56

image
57. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
57

image
58. Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.
58

image
59. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.
59

image
60. Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?
60

image
61. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
61

image
62. Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.
62

image
63. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
63

image
64. Za kijani kibivu.
64

image
65. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
65

image
66. Na chemchem mbili zinazo furika.
66

image
67. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
67

image
68. Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.
68

image
69. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
69

image
70. Humo wamo wanawake wema wazuri.
70

image
71. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
71

image
72. Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.
72

image
73. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
73

image
74. Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.
74

image
75. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
75

image
76. Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.
76

image
77. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
77

image
78. Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
78


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani