Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

53.Surat An-Najm


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa nyota inapo tua,
1

image
2. Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
1

image
3. Wala hatamki kwa matamanio.
3

image
4. Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
4

image
5. Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
5

image
6. Mwenye kutua, akatulia,
6

image
7. Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
7

image
8. Kisha akakaribia na akateremka.
8

image
9. Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
9

image
10. Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
10

image
11. Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
11

image
12. Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
12

image
13. Na akamwona mara nyingine,
13

image
14. Penye Mkunazi wa mwisho.
14

image
15. Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
15

image
16. Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
16

image
17. Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
17

image
18. Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
18

image
19. Je! Mmemuona Lata na Uzza?
19

image
20. Na Manaat, mwingine wa tatu?
20

image
21. Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
21

image
22. Huo ni mgawanyo wa dhulma!
22

image
23. Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
23

image
24. Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
24

image
25. Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
25

image
26. Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
26

image
27. Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
27

image
28. Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
28

image
29. Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
29

image
30. Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
30

image
31. Ni vya Mwenyezi Mungu vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, ili awalipe walio tenda ubaya kwa waliyo yatenda, na walio tenda mema awalipe mema.
31

image
32. Ambao wanajiepusha na madhambi makuu na vitendo vichafu, isipo kuwa makosa khafifu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mkunjufu wa maghfira, naye anakujueni sana tangu alipo kuumbeni kutoka kwenye ardhi, na mlipo kuwa mimba matumboni mwa mama zenu. Basi msijisifu usafi. Yeye anamjua sana mwenye kujikinga na maovu.
32

image
33. Je! Umemwona yule aliye geuka?
33

image
34. Na akatoa kidogo, kisha akajizuia?
34

image
35. Je! Anayo huyo ilimu ya ghaibu, basi ndio anaona?
35

image
36. Au hakuambiwa yaliyomo katika Vitabu vya Musa?
36

image
37. Na vya Ibrahimu aliye timiza ahadi?
37

image
38. Ya kwamba hakika nafsi iliyo beba madhambi haibebi madhambi ya mwengine?
38

image
39. Na ya kwamba hatapata mtu ila aliyo yafanya mwenyewe?
39

image
40. Na kwamba vitendo vyake vitaonekana?
40

image
41. Kisha ndio atalipwa malipo yake kwa ukamilifu.
41

image
42. Na kwamba kwao Mola wako Mlezi ndio mwisho.
42

image
43. Na kwamba Yeye ndiye anaye leta kicheko na kilio.
43

image
44. Na kwamba Yeye ndiye anaye fisha na kuhuisha.
44

image
45. Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
45

image
46. Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.
46

image
47. Na kwamba ni juu yake ufufuo mwengine.
47

image
48. Na kwamba ni Yeye ndiye anaye tosheleza na kukinaisha.
48

image
49. Na kwamba hakika Yeye ndiye Mola Mlezi wa nyota ya Shii'ra.
49

image
50. Na kwamba Yeye ndiye aliye waangamiza A'di wa kwanza,
50

image
51. Na Thamudi hakuwabakisha,
51

image
52. Na kabla yao kaumu ya Nuhu. Na hao hakika walikuwa ni madhaalimu zaidi, na waovu zaidi;
52

image
53. Na miji iliyo pinduliwa, ni Yeye aliye ipindua.
53

image
54. Vikaifunika vilivyo funika.
54

image
55. Basi neema gani ya Mola wako Mlezi unayo ifanyia shaka?
55

image
56. Hili ni Onyo katika maonyo yale yale ya zamani.
56

image
57. Kiyama kimekaribia!
57

image
58. Hapana wa kukifichua isipo kuwa Mwenyezi Mungu.
58

image
59. Je! Mnayastaajabia maneno haya?
59

image
60. Na mnacheka, wala hamlii?
60

image
61. Nanyi mmeghafilika?
61

image
62. Basi msujudieni Mwenyezi Mungu, na mumuabudu.
62
 


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani