Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

78.Surat An-Nabaa


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. WANAULIZANA nini?
1

image
2. Ile khabari kuu,
2

image
3. Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
3

image
4. La! Karibu watakuja jua.
4

image
5. Tena la! Karibu watakuja jua.
5

image
6. kaKwani hatukuifanya ardhi ma tandiko?
6

image
7. kama Na milima vigingi?
7

image
8. Na tukakuumbeni kwa jozi?
8

image
9. Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
9

image
10. Na tukaufanya usiku ni nguo?
10

image
11. Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
11

image
12. Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
12

image
13. Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
13

image
14. Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
14

image
15. Ili tutoe kwayo nafaka na mimea.
15

image
16.Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
16

image
17. Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
17

image
18. Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
18

image
19. Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango.
19

image
20. Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
20

image
21. Hakika Jahannamu inangojea!
21

image
22. Kwa walio asi ndio makaazi yao,
1

image
23. Wakae humo karne baada ya karne,
23

image
24. Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
24

image
25. Ila maji yamoto sana na usaha,
25

image
26. Ndio jaza muwafaka.
26

image
27. Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
27

image
28. Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
28

image
29. Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
29

image
30. Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
30

image
31. Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
31

image
32. Mabustani na mizabibu,
32

image
33. Na wake walio lingana nao,
33

image
34. Na bilauri zilizo jaa,
34

image
35. Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo,
35

image
36. Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
36

image
37. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
37

image
38. Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
38

image
39. Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi
39

image
40. Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo! 
40


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani