Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

79.Surat An-Naaziaat


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
1

image
2. Na kwa wanao toa kwa upole,
2

image
3. Na wanao ogelea,
3

image
4. Wakishindana mbio,
4

image
5. Wakidabiri mambo.
5

image
6. Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
6

image
7. Kifuate cha kufuatia.
7

image
8. Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
8

image
9. Macho yatainama chini,
9

image
10. Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
10

image
11. Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
11

image
12. Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
12

image
13. Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
13

image
14. Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
14

image
15. Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
15

image
16. Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
16

image
17. Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri
17

image
18. Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
18

image
19. Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
19

image
20. Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
20

image
21. Lakini aliikadhibisha na akaasi.
21

image
22. Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
22

image
23. Akakusanya watu akanadi.
23

image
24. Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
24

image
25. Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
25

image
26. Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
26

image
27. . Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
27

image
28. Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
28

image
29. Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake
29

image
30. Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
30

image
31. Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
31

image
32. Na milima akaisimamisha,
32

image
33. Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
33

image
34. Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
34

image
35. Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
35

image
36. Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
36

image
37. Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
37

image
38. Na akakhiari maisha ya dunia,
38

image
39. Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
39

image
40. Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
40

image
41. Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
41

image
42. Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
42

image
43. Una nini wewe hata uitaje?
43

image
44. Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
44

image
45. Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
45

image
46. Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
46


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani