Tarjuma ya Quran Tukufu kwa
kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua, 1

2. Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
2

3.
Wakishambulia wakati wa asubuhi, 3

4. Huku wakitimua vumbi, 4

5. Na wakijitoma kati ya kundi, 5

6.
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake
Mlezi! 6

7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa
hayo! 7

8. Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
8

9. Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
9

10. Na yakakusanywa yaliomo vifuani? 10

11.
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka
atakuwa na khabari zao wote! 11
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin
Al-Barwani
Ikiwa
una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com
Copyright � 22 August 1997, Sheikh
Ali Muhsin Al Barwani