Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

100.Surat Al-'Aadiyaat


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
1

image
2. Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
2

image
3. Wakishambulia wakati wa asubuhi,
3

image
4. Huku wakitimua vumbi,
4

image
5. Na wakijitoma kati ya kundi,
5

image
6. Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
6

image
7. Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
7

image
8. Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
8

image
9. Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
9

image
10. Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
10

image
11. Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
11


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani