Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

99.Surat Az-Zilzalah

 

image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
1

image
2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
2

image
3. Na mtu akasema: Ina nini?
3

image
4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.
4

image
5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

image
6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
6

image
7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
7

image
8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
8


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani