Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

56.Surat Al-Waaqia'h


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Litakapo tukia hilo Tukio
1

image
2. Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
1

image
3. Literemshalo linyanyualo,
3

image
4. Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
4

image
5. Na milima itapo sagwasagwa,
5

image
6. Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
6

image
7. Na nyinyi mtakuwa namna tatu:
7

image
8. Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
8

image
9. Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
9

image
10. Na wa mbele watakuwa mbele.
10

image
11. Hao ndio watakao karibishwa
11

image
12. Katika Bustani zenye neema.
12

image
13. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
13

image
14. Na wachache katika wa mwisho.
14

image
15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
15

image
16. Wakiviegemea wakielekeana.
16

image
17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
17

image
18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
18

image
19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
19

image
20. Na matunda wayapendayo,
20

image
21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
21

image
22. Na Mahurulaini,
22

image
23. Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
23

image
24. Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
24

image
25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
25

image
26. Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
26

image
27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
27

image
28. Katika mikunazi isiyo na miba,
28

image
29. Na migomba iliyo pangiliwa,
29

image
30. Na kivuli kilicho tanda,
30

image
31. Na maji yanayo miminika,
31

image
32. Na matunda mengi,
32

image
33. Hayatindikii wala hayakatazwi,
33

image
34. Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
34

image
35. Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
35

image
36. Na tutawafanya vijana,
36

image
37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
37

image
38. Kwa ajili ya watu wa kuliani.
38

image
39. Fungu kubwa katika wa mwanzo,
39

image
40. Na fungu kubwa katika wa mwisho.
40

image
41. Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
41

image
42. Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
42

image
43. Na kivuli cha moshi mweusi,
43

image
44. Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
44

image
45. Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
45

image
46. Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
46

image
47. Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
47

image
48. Au baba zetu wa zamani?
48

image
49. Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
49

image
50. Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
50

image
51. Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
51

image
52. Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
52

image
53. Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
53

image
54. Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
54

image
55. Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
55

image
56. Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
56

image
57. Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
57

image
58. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
58

image
59. Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
59

image
60. Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
60

image
61. Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
61

image
62. Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
62

image
63. Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
63

image
64. Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
64

image
65. Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
65

image
66. Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
66

image
67. Bali sisi tumenyimwa.
67

image
68. Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
68

image
69. Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
69

image
70. Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
70

image
71. Je! Mnauona moto mnao uwasha?
71

image
72. Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
72

image
73. Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
73

image
74. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
74

image
75. Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
75

image
76. Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
76

image
77. Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
77

image
78. Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
78

image
79. Hapana akigusaye ila walio takaswa.
79

image
80. Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
80

image
81. Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
81

image
82. Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
82

image
83. Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
83

image
84. Na nyinyi wakati huo mnatazama!
84

image
85. Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
85

image
86. Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
86

image
87. Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
87

image
88. Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
88

image
89. Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
89

image
90. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
90

image
91. Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
91

image
92. Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
92

image
93. Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
93

image
94. Na kutiwa Motoni.
94

image
95. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
95

image
96. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.
96


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani