Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

54.Surat Al-Qamar


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
1

image
2. Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
1

image
3. Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
3

image
4. Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
4

image
5. Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
5

image
6. Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
6

image
7. Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
7

image
8. Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
8

image
9. Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
9

image
10. Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
10

image
11. Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
11

image
12. Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
12

image
13. Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
13

image
14. Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
14

image
15. Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
15

image
16. Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
16

image
17. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
17

image
18. Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
18

image
19. Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
19

image
20. Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
20

image
21. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
21

image
22. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
22

image
23. Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
23

image
24. Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
24

image
25. Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
25

image
26. Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
26

image
27. Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
27

image
28. Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
28

image
29. Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
29

image
30. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
30

image
31. Hakika Sisi tuliwapelekea ukelele mmoja tu, wakawa kama mabuwa ya kujengea uwa.
31

image
32. Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kwa kukumbuka, lakini yupo akumbukaye?
32

image
33. Kaumu Lut'i nao waliwakadhibisha Waonyaji.
33

image
34. Hakika Sisi tukawapelekea kimbunga cha vijiwe, isipo kuwa wafuasi wa Lut'i. Hao tuliwaokoa karibu na alfajiri.
34

image
35. Kwa neema inayo toka kwetu. Hivyo ndivyo tumlipavyo anaye shukuru.
35

image
36. Na hakika yeye aliwaonya adhabu yetu; lakini wao waliyatilia shaka hayo maonyo.
36

image
37. Na walimtaka awape wageni wake. Tukayapofua macho yao, na tukawaambia: Onjeni basi adhabu na maonyo yangu!
37

image
38. Na iliwafikia wakati wa asubuhi adhabu yangu ya kuendelea.
38

image
39. Basi onjeni adhabu na maonyo yangu!<
39

image
40. Na hakika tumeisahilisha Qur'ani kuikumbuka. Lakini yupo anaye kumbuka?
40

image
41. Na Waonyaji waliwafikia watu wa Firauni.
41

image
42. Walizikadhibisha Ishara zetu zote, nasi tukawashika kama anavyo shika Mwenye nguvu Mwenye uweza.
42

image
43. Je! Makafiri wenu ni bora kuliko hao, au yameandikwa vitabuni kuwa nyinyi hamtiwi makosani?
43

image
44. Au ndio wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
44

image
45. Wingi wao huu utashindwa, na wao watasukumwa nyuma.
45

image
46. Bali Saa ya Kiyama ndio miadi yao, na Saa hiyo ni nzito zaidi na chungu zaidi.
46

image
47. Hakika wakosefu wamo katika upotofu na wazimu.
47

image
48. Siku watakapo kokotwa Motoni kifudifudi waambiwe: Onjeni mguso wa Jahannamu!
48

image
49. Kwa hakika Sisi tumekiumba kila kitu kwa kipimo.
49

image
50. Na amri yetu haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.
50

image
51. Na bila ya shaka tumekwisha waangamiza wenzenu. Lakini yupo anaye kumbuka?
51

image
52. Na kila jambo walilo lifanya limo vitabuni.
52

image
53. Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
53

image
54. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na mito.
54

image
55. Katika makalio ya haki kwa Mfalme Mwenye uweza.
55


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani