Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

68.Surat Al-Qalam


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
1

image
2. Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
2

image
3. Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
3

image
4. Na hakika wewe una tabia tukufu.
4

image
5. Karibu utaona, na wao wataona,
5

image
6. Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
6

image
7. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
7

image
8. Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
8

image
9. Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
9

image
10. Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
10

image
11. Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
11

image
12. Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
12

image
13. Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
13

image
14. Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
14

image
15. Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
15

image
16. Tutamtia kovu juu ya pua yake.
16

image
17. Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
17

image
18. Wala hawakusema: Mungu akipenda!
18

image
19. Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
19

image
20. Likawa kama usiku wa giza.
20

image
21. Asubuhi wakaitana.
21

image
22. Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
22

image
23. Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
23

image
24. Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
24

image
25. Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
25

image
26. Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
26

image
27. Bali tumenyimwa!
27

image
28. Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
28

image
29. Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
29

image
30. Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
30

image
31. Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
31

image
32. Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
32

image
33. Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
33

image
34. Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
34

image
35. Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
35

image
36. Mna nini? Mnahukumu vipi?
36

image
37. Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
37

image
38. Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
38

image
39. Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
39

image
40. Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
40

image
41. Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
41

image
42. Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
42

image
43. Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima
43

image
44. Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
44

image
45. Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
45

image
46. Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
46

image
47. Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
47

image
48. Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
48

image
49. Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
49

image
50. Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
50

image
51. Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
51

image
52. Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote. 
52


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani