Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

101.Surat Al-Qaaria'h


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Inayo gonga!
1

image
2. Nini Inayo gonga?
2

image
3. Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
3

image
4. Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
4

image
5. Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
5

image
6. Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
6

image
7. Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
7

image
8. Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
8

image
9. Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
9

image
10. Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
10

image
11. Ni Moto mkali!
11


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani