Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

73.Surat Al-Muzzammil


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Ewe uliye jifunika!
1

image
2. Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
2

image
3. Nusu yake, au ipunguze kidogo.
3

image
4. Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
4

image
5. ka Hakika Sisi tutakuteremshia uli nzito.
5

image
6. Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
6

image
7. Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
7

image
8. Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
8

image
9. Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
9

image
10. Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
10

image
11. Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
11

image
12. Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
12

image
13. Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
13

image
14. Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga.
14

image
15. Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
15

image
16. Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
16

image
17. Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
17

image
18. Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
18

image
19. Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
19

image
image
20. Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
20


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani