Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

83.Surat Al-Mutaffifeen


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Ole wao hao wapunjao!
1

image
2. Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
2

image
3. Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
3

image
4. Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
4

image
5. Katika Siku iliyo kuu,
5

image
6. Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
6

image
7. Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
7

image
8. Unajua nini Sijjin?
8

image
9. Kitabu kilicho andikwa.
9

image
10. Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
10

image
11. Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
11

image
12. Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
12

image
13. Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
13

image
14. Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
14

image
15. Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
15

image
16. Kisha wataingia Motoni!
16

image
17. Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
17

image
18. Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
18

image
19. Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
19

image
20. Kitabu kilicho andikwa.
20

image
21. Wanakishuhudia walio karibishwa.
21

image
22. Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
22

image
23. Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
23

image
24. Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
24

image
25. Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
25

image
26. Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
26

image
27. Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
27

image
28. Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
28

image
29. Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
29

image
30 Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
30

image
31. Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
31

image
32. Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
32

image
33. Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
33

image
34. Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
34

image
35. Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
35

image
36. Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
36

Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani