Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahi li

77.Surat Al-Mursalaat


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
1

image
2. Na zinazo vuma kwa kasi!
2

image
3. Na zikaeneza maeneo yote!
image
4. Na zinazo farikisha zikatawanya!
4

image
5. Na zinazo peleka mawaidha!
5

image
6. Kwa kuudhuru au kuonya,
6

image
7. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
7

image
8. Wakati nyota zitakapo futwa,
8

image
9. Na mbingu zitakapo pasuliwa,
9

image
10. Na milima itakapo peperushwa,
10

image
11. Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
11

image
12. Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
12

image
13. Kwa siku ya kupambanua!
13

image
14. Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
14

image
15. Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
16

image
16. Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
16

image
17. Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
18

image
18. Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
18

image
19. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
19

image
20. Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
20

image
21. Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
21

image
22. Mpaka muda maalumu?
22

image
23. Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
23

image
24. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
24

image
25. Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
25

image
26. Walio hai na maiti?
26

image
27. Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
27

image
28. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
28

image
29. Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
29

image
30. Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
30

image
31. Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

 
  image
32. Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

 
image
33. Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

 
  image
34. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

 
  image
35. Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

 
  image
36. Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

 
  image
37. Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

 
  image
38. Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

 
  image
39. kiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

 
  image
40. Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

 
  image
41. Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
41

image
42. Na matunda wanayo yapenda,
42

image
43. Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
43

image
44. Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
44

image
45. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
45

image
46. Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
46

image
47. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
47

image
48. Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
48

image
49. Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
49

image
50. Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
50


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani