Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

70.Surat Al-Maarij


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
1

image
2. Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia
2

image
3. Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
3

image
4. Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
4

image
5. Basi subiri kwa subira njema.Hakika wao wanaiona iko mbali,
5

image
6. Hakika wao wanaiona iko mbali,
6

image
7. Na Sisi tunaiona iko karibu.
7

image
8. Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
8

image
9. Na milima itakuwa kama sufi.
9

image
10. Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
10

image
11. Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
11

image
12. Na mkewe, na nduguye,
12

image
13. Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
13

image
14. Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
14

image
15. La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
15

image
16. Unao babua ngozi ya kichwa!
16

image
17. Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
17

image
18. Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
18

image
19. Hakika mtu ameumbwa na papara.
19

image
20. Inapo mgusa shari hupapatika.
20

image
21. Na inapo mgusa kheri huizuilia.
21

image
22. Isipo kuwa wanao sali,
22

image
23. Ambao wanadumisha Sala zao,
23

image
24. Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
24

image
25. Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
25

image
26. Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
26

image
27. Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
27

image
28. Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
28

image
29. Na ambao wanahifadhi tupu zao.
29

image
30. Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi
30

image
31. Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka.
31

image
32. Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao,
32

image
33. Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao,
33

image
34. Na ambao wanazihifadhi Sala zao.
34

image
35. Hao ndio watakao hishimiwa Peponi.
35

image
36. Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu?
36

image
37. Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto!
37

image
38. Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema?
38

image
39. La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua.
39

image
40. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza
40

image
41. Kuwabadili kwa walio bora kuliko wao; na Sisi hatushindwi.
41

image
42. Basi waache wapige porojo na wacheze, mpaka wakutane na siku yao wanayo ahidiwa,
42

image
43. Siku watakapotoka makaburini kwa upesi kama kwamba wanakimbilia mfundo,
43

image
44. Macho yao yatainama, fedheha itawafunika. Hiyo ndiyo Siku waliyo kuwa wakiahidiwa.
44


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani