Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

92.Surat Al-Layl


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa usiku unapo funika!
1

image
2. Na mchana unapo dhihiri!
2

image
3. Na kwa Aliye umba dume na jike!
3

image
4. Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.
4

image
5. Ama mwenye kutoa na akamchamngu,
5

image
6. Na akaliwafiki lilio jema,
6

image
7. Tutamsahilishia yawe mepesi.
7

image
8. Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,
8

image
9. Na akakanusha lilio jema,
9

image
10. Tutamsahilishia yawe mazito!
10

image
11. Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?
11

image
12. Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.
1

image
13. Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.
13

image
14. Basi nakuonyeni na Moto unao waka!
14

image
15. Hatauingia ila mwovu kabisa!
15

image
16. Anaye kadhibisha na kupa mgongo.
16

image
17. Na mchamngu ataepushwa nao,
17

image
18. Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.
18

image
19. Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.
19

image
20. Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.
20

image
21. Naye atakuja ridhika!
21


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani