Tarjuma ya Quran Tukufu kwa
kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Itapo chanika mbingu, 1

2. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa
kumsikiliza, 2

3. Na ardhi itakapo tanuliwa, 3

4. Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
4

5. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa
kumsikiliza, 5

6. Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi
kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta. 6

7. Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
7

8. Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi, 8

9. Na arudi kwa ahali zake na furaha. 9

10. Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya
mgongo wake, 10

11.
Basi huyo ataomba kuteketea. 11

12. Na ataingia Motoni. 12

13.
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
13

14.
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena. 14

15.
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
15

16.
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
16

17. Na kwa usiku na unavyo vikusanya, 17

18. Na kwa mwezi unapo pevuka, 18

19.
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka! 19

20.
Basi wana nini hawaamini? 20

21. Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu? 21

22.
Bali walio kufuru wanakanusha tu. 22

23. Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
23

24.
Basi wabashirie adhabu chungu! 24

25.
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao
watakuwa na ujira usio malizika. 25
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii
qurani-tukufu@geocities.com
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali
Muhsin Al Barwani