Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

84.Surat al-Inshiqaaq


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Itapo chanika mbingu,
1

image
2. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
2

image
3. Na ardhi itakapo tanuliwa,
3

image
4. Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
4

image
5. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
5

image
6. Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
6

image
7. Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
7

image
8. Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
8

image
9. Na arudi kwa ahali zake na furaha.
9

image
10. Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
10

image
11. Basi huyo ataomba kuteketea.
11

image
12. Na ataingia Motoni.
12

image
13. Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
13

image
14. Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
14

image
15. Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
15

image
16. Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
16

image
17. Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
17

image
18. Na kwa mwezi unapo pevuka,
18

image
19. Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
19

image
20. Basi wana nini hawaamini?
20

image
21. Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
21

image
22. Bali walio kufuru wanakanusha tu.
22

image
23. Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
23

image
24. Basi wabashirie adhabu chungu!
24

image
25. Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
25


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani