Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

76.Surat Al-Insan


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
1

image
2. Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
2

image
3. Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
3

image
4. kika HaSisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
4

image
5. Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
5

image
6. Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
6

image
7. Wanatimiza ahadi,na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
7

image
8. Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
8

image
9. Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
9

image
10. Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
10

image
11. Basi Mwenyna raha na furahaezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha.
11

image
12. Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
12

image
13 Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
13

image
14 Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
14

image
15 Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
15

image
16 Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
16

image
17 Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
17

image
18 Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
18

image
19 Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
19

image
20 Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
20

image
21 Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
21

image
22 Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
22

image
23 Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
23

image
24 Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
24

image
25 Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
25

image
26 Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
26

image
27 Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
27

image
28 Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
28

image
29 Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
29

image
30 Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
30

image
31 Humuingiza amtakaye katika rehema yake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iliyo chungu. 
31


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani