Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

82.Surat Al-Infitaar


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Mbingu itapo chanika,
1

image
2. Na nyota zitapo tawanyika,
2

image
3. Na bahari zitakapo pasuliwa,
3

image
4. Na makaburi yatapo fukuliwa,
4

image
5. Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
5

image
6. Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
6

image
7. Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
7

image
8. Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
8

image
9. Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
9

image
10. Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
10

image
11. Waandishi wenye hishima,
11

image
12. Wanayajua mnayo yatenda.
12

image
13. Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
13

image
14. Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
14

image
15. Wataingia humo Siku ya Malipo.
15

image
16. Na hawatoacha kuwamo humo.
16

image
17. Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
17

image
18. Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
18

image
19. Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
19


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani