Tarjuma ya Quran Tukufu kwa
kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Ole wake kila safihi, msengenyaji! 1

2. Aliye kusanya mali na kuyahisabu. 2

3.
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
3

4. Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama. 4

5. Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama? 5

6. Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa. 6

7. Ambao unapanda nyoyoni. 7

8. Hakika huo utafungiwa nao 8

9. Kwenye nguzo zilio nyooshwa. 9
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin
Al-Barwani
Ikiwa
una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com
Copyright � 22 August 1997, Sheikh
Ali Muhsin Al Barwani