Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

104.Surat Al-Humazah


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Ole wake kila safihi, msengenyaji!
1

image
2. Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
2

image
3. Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
3

image
4. Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
4

image
5. Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
5

image
6. Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
6

image
7. Ambao unapanda nyoyoni.
7

image
8. Hakika huo utafungiwa nao
8

image
9. Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
9


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani