Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

15.Surat Al-Hijr


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 0

image
15. Alif Lam Ra. (A.L.R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha. 1

image
2. HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu. 2

image
3. Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua. 3

image
4. Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu. 4

image
5. Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa. 5

image
6. Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu. 6

image
7. Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli? 7

image
8. Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula. 8

image
9. Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda. 9

image
10. Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo. 10

image
11. Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli. 11

image
12. Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu. 12

image
13. Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale. 13

image
14. Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda, 14

image
15. Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa. 15

image
16. Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia. 16

image
17. Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye. 17

image
18. Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana. 18

image
19. Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake. 19

image
20. Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku. 20

image
21. Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu. 21

image
22. Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka. 22

image
23. Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi. 23

image
24. Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua waliotaakhari. 24

image
25. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi. 25

image
26. Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura. 26

image
27. Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto. 27

image
28. Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura. 28

image
29. Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia. 29

image
30. Basi Malaika wote pamoja walimsujudia, 30

image
31. Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu. 31

image
32. (Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu? 32

image
33. Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unaotoa sauti, unao tokana na matope yenye sura. 33

image
34. (Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni! 34

image
35. Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo. 35

image
36. Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapofufuliwa. 36

image
37. (Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula 37

image
38. Mpaka siku ya wakati maalumu. 38

image
39. Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote, 39

image
40. Ila waja wako walio safika. 40

image
41. Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka. 41

image
42. Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata. 42

image
43. Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote. 43

image
44. Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa. 44

image
45. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem. 45

image
46. (Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani. 46

image
47. Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana. 47

image
48. Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo. 48

image
49. Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. 49

image
50. Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu! 50

image
51. Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim. 51

image
52. Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni. 52

image
53. Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi. 53

image
54. Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria? 54

image
55. Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa. 55

image
56. Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea? 56

image
57. Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe? 57

image
58. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu! 58

image
59. Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote. 59

image
60. Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma. 60

image
61. Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i, 61

image
62. Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana. 62

image
63. Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka. 63

image
64. Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli. 64

image
65. Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao,wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa. 65

image
66. Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali. 66

image
67. Na wakaja watu wa mji ule nao furahani. 67

image
68. Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe. 68

image
69. Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi. 69

image
70. Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote? 70

image
71. Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji. 71

image
72. Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo. 72

image
73. Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa. 73

image
74. Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni. 74

image
75. Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi. 75

image
76. Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa. 76

image
77. Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini. 77

image
78. Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini. 78

image
79. Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia iliowazi. 79

image
80. Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume. 80

image
81. Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza. 81

image
82. Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani. 82

image
83. Basi ukelele ukawatwaa asubuhi. 83

image
84. Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma. 84

image
85. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri. 85

image
86. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi. 86

image
87. Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu. 87

image
88. Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini. 88

image
89. Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha. 89

image
90. Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa, 90

image
91. Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande. 91

image
92. Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote. 92

image
93. Kwa waliyo kuwa wakiyatenda. 93

image
94. Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina. 94

image
95. Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli. 95

image
96. Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine.Basi, watakuja jua! 96

image
97. Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo. 97

image
98. Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanaomsujudia. 98

image
99. Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.  99


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani