Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

69.Surat Al-Haaqqah

 

image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Tukio la haki.
1

image
2. Nini hilo Tukio la haki?
2

image
3. Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
3

image
4. Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
4

image
5. Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
5

image
6. Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
6

image
7. Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
7

image
8. Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
8

image
9. Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
9

image
10. Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
10

image
11. Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
11

image
12. Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
12

image
.13 Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
13

image
14. Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
14

image
15. Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
15

image
16. Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
16

image
17. Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
17

image
18. Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
18

image
19. Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
19

image
20. Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
20

image
21. Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
21

image
22. Katika Bustani ya juu,
22

image
23. Matunda yake yakaribu.
23

image
24. Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
24

image
25. Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
25

image
26. Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
26

image
27. Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
27

image
28. Mali yangu hayakunifaa kitu.
28

image
29. Madaraka yangu yamenipotea.
29

image
30. (Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
30

image
31. Kisha mtupeni Motoni!
31

image
32. Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!
32

image
33. Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,
33

image
34. Wala hahimizi kulisha masikini.
34

image
35. Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,
35

image
36. Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.
36

image
37. Chakula hicho hawakili ila wakosefu.
37

image
38. Basi naapa kwa mnavyo viona,
38

image
39. Na msivyo viona,
39

image
40. Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.
40

image
41. Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.
41

image
42. Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.
42

image
43. Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
43

image
44. Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,
44

image
45. Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,
45

image
46. Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!
46

image
47. Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.
47

image
48. Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.
48

image
49. Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
49

image
50. Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.
50

image
51. Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.
51

image
52. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.
52


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani