Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

88.Surat Al-Ghaashiyah


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
1

image
2. Siku hiyo nyuso zitainama,
2

image
3. Zikifanya kazi, nazo taabani.
3

image
4. Ziingie katika Moto unao waka
4

image
5. Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
5

image
6. Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
6

image
7. Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
7

image
8. Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
8

image
9. Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
9

image
10. Katika Bustani ya juu.
10

image
11. Hawatasikia humo upuuzi.Humo imo chemchem inayo miminika.
11

image
12. Humo imo chemchem inayo miminika.
12

image
13. Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
13

image
14. Na bilauri zilizo pangwa,
14

image
15. Na matakia safu safu,
15

image
16. Na mazulia yaliyo tandikwa.
16

image
17. Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
17

image
18. Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
18

image
19. Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
19

image
20. Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
20

image
21. Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
21

image
22. Wewe si mwenye kuwatawalia.
22

image
23. Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
23

image
24.Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa
24

image
25. Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
25

image
26. Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
26


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani