Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

89.Surat Al-Fajr


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa alfajiri,
1

image
2. Na kwa masiku kumi,
2

image
3. Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
3

image
4. Na kwa usiku unapo pita,
4

image
5. Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
5

image
6. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
6

image
7. Wa Iram, wenye majumba marefu?
7

image
8. Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
8

image
9. Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
9

image
10. Na Firauni mwenye vigingi?
10

image
11. Ambao walifanya jeuri katika nchi?
11

image
12. Wakakithirisha humo ufisadi?
12

image
13. Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
13

image
14. Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
14

image
15. Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
15

image
16. Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
16

image
17. Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
17

image
18. Wala hamhimizani kulisha masikini;
18

image
19. Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
19

image
20. Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
20

image
21. Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
21

image
22. Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
22

image
23. Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
23

image
24. Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
24

image
25. Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
25

image
26. Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
26

image
27. Ewe nafsi iliyo tua!
27

image
28. Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
28

image
29. Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
29

image
30. Na ingia katika Pepo yangu.
30


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani