Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

1.Surat al-Faatiha


image
1. KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

image
2. Sifa njema zote ni za Mwenyeezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;

image
3. Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;

image
4. Mwenye kumiliki siku ya malipo.

 
image
5. Wewe tu tunakuabudu, na wewe tu tunakuomba msaada.

image
6. Tuongoe njia iliyonyooka.

image
7. Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani