Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

85.Surat Al-Buruuj


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa mbingu yenye Buruji! 1

image
2. Na kwa siku iliyo ahidiwa!
2

image
3. Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
3

image
4. Wameangamizwa watu wa makhandaki
4

image
5. Yenye moto wenye kuni nyingi,
5

image
6. Walipo kuwa wamekaa hapo,
6

image
7. Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
7

image
8. Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
8

image
9. Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
9

image
10. Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
10

image
11. Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
11

image
12. Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
12

image
13. Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
13

image
14. Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
14

image
15. Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
15

image
16. Atendaye ayatakayo.
16

image
17. Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
17

image
18. Ya Firauni na Thamudi?
18

image
19. Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
19

image
20. Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
20

image
21. Bali hii ni Qur'ani tukufu
21

image
22. Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
22


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani