Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

90.Surat al-Balad


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa Mji huu!
1

image
2.Nawe unaukaa Mji huu.
2

image
3. Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
3

image
4. Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
4

image
5. Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
5

image
6. Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
6

image
7. Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
7

image
8. Kwani hatukumpa macho mawili?
8

image
9. Na ulimi, na midomo miwili?
9

image
10. Na tukambainishia zote njia mbili?
10

image
11. Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
11

image
12. Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
12

image
13. Kumkomboa mtumwa;
13

image
14. Au kumlisha siku ya njaa
14

image
15. Yatima aliye jamaa,
15

image
16. Au masikini aliye vumbini.
16

image
17. Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
17

image
18. Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
18

image
19. Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
19

image
20. Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
20


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani