Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU
MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

1. Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
1

2. Amemuumba binaadamu kwa tone la damu, 2

3. Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
3

4. Ambaye amefundisha kwa kalamu. 4

5. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui. 5

6. Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri 6

7. Akijiona katajirika. 7

8. Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo. 8

9. Umemwona yule anaye mkataza 9

10 . Mja anapo sali? 10

11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu? 11

12. Au anaamrisha uchamngu? 12

13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
13

14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona? 14

15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la
nywele! 15

16. Shungi la uwongo, lenye makosa! 16

17. Basi na awaite wenzake! 17

18. Nasi tutawaita Mazabania! 18

19. Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee! 19
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin
Al-Barwani
Ikiwa
una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii [email protected]
Copyright � 22 August 1997, Sheikh
Ali Muhsin Al Barwani