Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

96.Surat Al-'Alaq


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
1

image
2. Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
2

image
3. Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
3

image
4. Ambaye amefundisha kwa kalamu.
4

image
5. Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
5

image
6. Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
6

image
7. Akijiona katajirika.
7

image
8. Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
8

image
9. Umemwona yule anaye mkataza
9

image
10 . Mja anapo sali?
10

image
11. Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
11

image
12. Au anaamrisha uchamngu?
12

image
13. Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
13

image
14. Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
14

image
15. Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
15

image
16. Shungi la uwongo, lenye makosa!
16

image
17. Basi na awaite wenzake!
17

image
18. Nasi tutawaita Mazabania!
18

image
19. Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
19


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii [email protected] 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani