Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

87.Surat Al-A'alaa


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
1

image
2. Aliye umba, na akaweka sawa,
2

image
3. Na ambaye amekadiria na akaongoa,
3

image
4. Na aliye otesha malisho,
4

image
5. Kisha akayafanya makavu, meusi.
5

image
6. Tutakusomesha wala hutasahau,
6

image
7. Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
7

image
8. Na tutakusahilishia yawe mepesi.
8

image
9. Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
9

image
10. Atakumbuka mwenye kuogopa.
10

image
11. Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
11

image
12. Ambaye atauingia Moto mkubwa.
12

image
13. Tena humo hatakufa wala hawi hai.
13

image
14. Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
14

image
15. Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
15

image
16. Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
16

image
17. Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
17

image
18. Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
18

image
19. Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
19


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani