Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

23.Surat Al-Mu'minun

 

image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
1

image
2. Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
2

image
3. Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
3

image
4. Na ambao wanatoa Zaka,
4

image
5. Na ambao wanazilinda tupu zao,
5

image
6. Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
6

image
7. Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
7

image
8. Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
8

image
9. Na ambao Sala zao wanazihifadhi
9

image
10. Hao ndio warithi,
10

image
11. Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
11

image
12. Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
12

image
13. Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
13

image
14. Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
14

image
15. Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
15

image
16. Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
16

image
17. Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
17

image
18. Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
18

image
19. Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
19

image
20. Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
20

image
21. Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
21

image
22. Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
22

image
23. Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
23

image
24. Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
24

image
25. Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
25

image
26. Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
26

image
27. Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
27

image
28. Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
28

image
29. Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
29

image
30. Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
30

image
31. Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
31

image
32. Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
32

image
33. Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
33

image
34. Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
34

image
35. Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
35

image
36. Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.
36

image
37. Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Mwenyezi Mungu uwongo, wala sisi sio wa kumuamini.
37

image
38. Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
38

image
39. (Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
39

image
40. Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
40

image
41. Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
41

image
42. Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
42

image
43. Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
43

image
44. Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
44

image
45. Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
45

image
46. Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
46

image
47. Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
47

image
48. Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
48

image
49. Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
49

image
50. Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.
50

image
51. Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda.
51

image
52. Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi.
52

image
53. Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo.
53

image
54. Basi waache katika ghafla yao kwa muda.
54

image
55. Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto
55

image
56. Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui.
56

image
57. Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea,
57

image
58. Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini,
58

image
59. Na wale ambao Mola wao Mlezi hawamshirikishi,
59

image
60. Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinagopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,
60

image
61. Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
61

image
62. Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa.
62

image
63. Lakini nyoyo zao zimeghafilika na hayo, na wanavyo vitendo vinginevyo wanavyo vifanya.
63

image
64. Hata tutakapo watia katika adhabu wale walio dekezwa kwa starehe kati yao, hapo ndipo watapo yayatika.
64

image
65. Msiyayatike leo! Hakika nyinyi hamtanusurika nasi.
65

image
66. Hakika zilikuwa Aya zangu mkisomewa, nanyi mkirudi nyuma juu ya visigino vyenu,
66

image
67. Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
67

image
68. Je, hawakuifikiri kauli, au yamewajia yasiyo wafikia baba zao wa zamani?
68

image
69. Au hawakumjua Mtume wao, ndio maana wanamkataa?
69

image
70. Au wanasema: Ana wazimu? Bali amewajia kwa Haki, na wengi wao wanaichukia Haki.
70

image
71. Na lau kuwa Haki ingeli fuata matamanio yao, basi zingeli haribika mbingu na ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga mbali na ukumbusho wao.
71

image
72. Au unawaomba ujira? Lakini ujira wa Mola wako Mlezi ni bora, na Yeye ndiye Mbora wa wanao ruzuku.
72

image
73. Na kwa yakini wewe unawaita kwenye Njia Iliyo Nyooka.
73

image
74. Na hakika wale wasio iamini Akhera wanajitenga na Njia hiyo.
74

image
75. Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
75

image
76. Na hakika tuliwatia adhabu kali; lakini hawakuelekea kwa Mola wao Mlezi wala hawakunyenyekea.
76

image
77. Mpaka tulipo wafungulia mlango wa adhabu kali, hapo ndipo wakawa wenye kukata tamaa.
77

image
78. Na Yeye ndiye aliye kuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni kuchache mno kushukuru kwenu.
78

image
79. Na Yeye ndiye aliye kuenezeni katika ardhi, na kwake Yeye mtakusanywa.
79

image
80. Na Yeye ndiye anaye huisha na kufisha, na yake Yeye mabadiliko ya usiku na mchana. Basi je! Hamfahamu?
80

image
81. Bali wanasema kama walivyo sema watu wa kwanza.
81

image
82. Walisema: Je! Tukisha kufa tukawa udongo na mifupa ndio tutafufuliwa?
82

image
83. Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni visa vya uwongo vya watu wa zamani.
83

image
84. Sema: Ni ya nani ardhi na viliomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?
84

image
85. Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu! Sema: Basi, je, hamkumbuki?
85

image
86. Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu saba na Mola Mlezi wa A'rshi Kuu?
86

image
87. Watasema: Ni vya Mwenyezi Mungu. Sema: Basi je, hamwogopi?
87

image
88. Sema: Ni nani mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu, naye ndiye anaye linda, wala hakilindwi asicho taka, kama mnajua?
88

image
89. Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?
89

image
90. Bali tumewaletea Haki, na kwa yakini hao ni waongo.
90

image
91. Mwenyezi Mungu hana mwana yeyote, wala hanaye mungu mwengine. Inge kuwa hivyo basi kila mungu angeli chukua alivyo umba, na baadhi yao wangeli washinda wengine. Mwenyezi Mungu ameepukana na sifa wanazo msifu.
91

image
92. Mjuzi wa siri na dhaahiri, na ametukuka juu ya hayo wanayo mshirikisha nayo.
92

image
93. Sema: Mola wangu Mlezi! Ukinionyesha adhabu waliyo ahidiwa,
93

image
94. Mola wangu Mlezi! Usinijaalie katika watu madhaalimu hao.
94

image
95. Na hakika Sisi ni waweza wa kukuonyeshsa tuliyo waahidi.
95

image
96. Kinga maovu kwa kutenda yaliyo mema zaidi. Sisi tunajua wayasemayo.
96

image
97. Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani.
97

image
98. Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.
98

image
99. Mpaka yanapo mfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe.
99

image
100. Ili nitende mema sasa badala ya yale niliyo yaacha. Wapi! Hii ni kauli aisemayo yeye tu. Na nyuma yao kipo kizuizi mpaka siku watapo fufuliwa.
100

image
101. Basi litapo pulizwa baragumu hapo hautakuwapo ujamaa baina yao siku hiyo, wala hawataulizana.
101

image
102. Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa.
102

image
103. Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia khasarani nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu.
103

image
104. Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana.
104

image
105. Je! Hazikuwa Aya zangu mkisomewa, na nyinyi mkizikanusha?
105

image
106. Mola wetu Mlezi! Tulizidiwa na uovu wetu na tukawa watu tulio potea.
106

image
107. Mola wetu Mlezi! Tutoe humu Motoni. Na tufanyapo tena basi kweli sisi ni wenye kudhulumu.
107

image
108. Atasema Mwenyezi Mungu: Tokomeeni humo, wala msinisemeze.
108

image
109. Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
109

image
110. Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
110

image
111. Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
111

image
112. Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
112

image
113. Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
113

image
114. Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
114

image
115. Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
115

image
116. Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
116

image
117. Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
117

image
118. Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.
118


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright © 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani