Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

93.Surat Adh-Dhuhaa


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Naapa kwa mchana!
1

image
2. Na kwa usiku unapo tanda!
2

image
3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
3

image
4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko ulio tangulia.
4

image
5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
5

image
6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
6

image
7. Na akakukuta umepotea akakuongoa?
1

image
8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
8

image
9. Basi yatima usimwonee!
9

image
10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
10

image
11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
11


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani