Tarjuma ya Quran Tukufu kwa
kiswahili

KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

1. Naapa kwa mchana! 1

2. Na kwa usiku unapo tanda! 2

3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
3

4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako
kuliko ulio tangulia. 4

5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike. 5

6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi? 6

7. Na akakukuta umepotea akakuongoa? 1

8.
Akakukuta mhitaji akakutosheleza? 8

9. Basi yatima usimwonee! 9

10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie! 10

11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie. 11
Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin
Al-Barwani
Ikiwa
una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com
Copyright � 22 August 1997, Sheikh
Ali Muhsin Al Barwani