Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

51.Surat Adh-Dhaariyaat


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
1

image
2. Na zinazo beba mizigo,
1

image
3. Na zinazo kwenda kwa wepesi.
3

image
4. Na zinazo gawanya kwa amri,
4

image
5. Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
5

image
6. Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
6

image
7. Naapa kwa mbingu zenye njia,
7

image
8. Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
8

image
9. Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
9

image
10. Wazushi wameangamizwa.
10

image
11. Ambao wameghafilika katika ujinga.
11

image
12. Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
12

image
13. Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
13

image
14. Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
14

image
15. Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
15

image
16. Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
16

image
17. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
17

image
18. Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
18

image
19. Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
19

image
20. Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
20

image
21. Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
21

image
22. Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
22

image
23. Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
23

image
24. Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
24

image
25. Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
25

image
26. Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
26

image
27. Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
27

image
28. Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
28

image
29. Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
29

image
30. Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
30

image
31. AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
31

image
32. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
32

image
33. Tuwatupie mawe ya udongo,
33

image
34. Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
34

image
35. Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
35

image
36. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
36

image
37. Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
37

image
38. Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
38

image
39. Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
39

image
40. Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
40

image
41. Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
41

image
42. Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
42

image
43. Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
43

image
44. Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
44

image
45. Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
45

image
46. Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
46

image
47. Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
47

image
48. Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
48

image
49. Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
49

image
50. Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
50

image
51. Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
51

image
52. Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
52

image
53. Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
53

image
54. Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
54

image
55. Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
55

image
56. Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
56

image
57. Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
57

image
58. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
58

image
59. Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
59

image
60. Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.
60


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani