Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

44.Surat Ad-Dukhaan


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. H'a Mim
1

image
2. Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
2

image
3. Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
3

image
4. Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
4

image
5. Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
5

image
6. Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
6

image
7. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
7

image
8. Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
8

image
9. Lakini wao wanacheza katika shaka.
9

image
10. Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
10

image
11. Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
11

image
12. Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
12

image
13. Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
13

image
14. Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
14

image
15. Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
15

image
16. Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
16

image
17. Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
17

image
18. Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
18

image
19. Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
19

image
20. Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
20

image
21. Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
21

image
22. Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
22

image
23. Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
23

image
24. Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
24

image
25. Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
25

image
26. Na mimea na vyeo vitukufu!
26

image
27. Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
27

image
28. Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
28

image
29. La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
29

image
30. Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
30

image
31. Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
31

image
32. Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
32

image
33. Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
33

image
34. Hakika hawa wanasema:
34

image
35. Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
35

image
36. Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
36

image
37. Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
37

image
38. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
38

image
39. Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
39

image
40. Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
40

image
41. Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
41

image
42. Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
42

image
43. Hakika Mti wa Zaqqum,
43

image
44. Ni chakula cha mwenye dhambi.
44

image
45. Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
45

image
46. Kama kutokota kwa maji ya moto.
46

image
47. (Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
47

image
48. Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
48

image
49. Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
49

image
50. Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
50

image
51. Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
51

image
52. Katika mabustani na chemchem,
52

image
53. Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
53

image
54. Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
54

image
55. Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
55

image
56. Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
56

image
57. Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
57

image
58. Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
58

image
59. Ngoja tu, na wao wangoje pia.
59


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani