Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

75.Surat Al-Qiyamah


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1.Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
1

image
2.Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
2

image
3.Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
3

image
4.Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
4

image
5.Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
5

image
6.Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
6

image
7. Basi jicho litapo dawaa,
7

image
8.Na mwezi utapo patwa,
8

image
9.Na likakusanywa jua na mwezi,
9

image
10.Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
10

image
11.La! Hapana pa kukimbilia!
11

image
12.Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
12

image
13.Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
13

image
14. Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
14

image
15.Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
15

image
16. Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
16

image
17.Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
17

image
18. Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
18

image
19.Kisha ni juu yetu kuubainisha.
19

image
20.Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
20

image
21.Na mnaacha maisha ya Akhera.
21

image
22. Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
22

image
23.Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
23

image
24.Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
24

image
25.Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
25

image
26.La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
26

image
27. Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
27

image
28. Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
28

image
29.Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
29

image
30.Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
30

image
31.Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
31

image
32.Bali alikanusha, na akageuka.
32

image
33.Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
33

image
34.Ole wako, ole wako!
34

image
35.Kisha Ole wako, ole wako!
35

image
36. Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
36

image
37.Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
37

image
38.Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
38

image
39.Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
39

image
40. Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
40


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani