Mambo yanayoweza kutoa udhu wako


image



Post hii itakufundisha mambo ambayo yanabatilisha udhu.

Udhu unaweza kuharibika kwa sababu ya Moja kati ya mambo yafuatayo:-

  1. Kutokwa na upepo (kujamba)
  2. Kulala ulalaji usio wa kukaa
  3. Kutokwa na haja ndogo (mkojo)
  4. Kutokwa na haja kubwa au ndogo
  5. Kuzimia
  6. Kutokwa na hedhi
  7. Kutokwa na madii
  8. Kutokwa na madii
  9. Kutokwa na akili kwa kulewa ama maradhi
  10. Kutokwa na damu ya ugonjwa.

 

KUSINZIA HAKUHARIBU UDHU

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {كَانَ أَصْحَابُ رَسُولِ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏‏عَلَى عَهْدِهِ‏ يَنْتَظِرُونَ اَلْعِشَاءَ حَتَّى تَخْفِقَ رُؤُوسُهُمْ، ثُمَّ يُصَلُّونَ وَلَا يَتَوَضَّئُونَ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ

وَأَصْلُهُ فِي مُسْلِمٍ

 

Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Maswahaba wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), katika zama zake (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) walikuwa wakingojea Swalaah ya ‘Ishaa hadi wanainamisha chini vichwa vyao (kwa kusinzia), kisha wanaswali bila kutawadha upya[3].” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Ad-Daaruqutwniy]

 

 

DAMU YA UGONJWA INAHARIBU UDHU

وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {جَاءَتْ فَاطِمَةُ بِنْتُ أَبِي حُبَيْشٍ إِلَى اَلنَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنِّي اِمْرَأَةٌ أُسْتَحَاضُ فَلَا أَطْهُرُ، أَفَأَدَعُ اَلصَّلَاةَ؟ قَالَ: "لَا.‏ إِنَّمَا ذَلِكَ عِرْقٌ، وَلَيْسَ بِحَيْضٍ، فَإِذَا أَقْبَلَتْ حَيْضَتُكِ فَدَعِي اَلصَّلَاةَ، وَإِذَا أَدْبَرَتْ فَاغْسِلِي عَنْكِ اَلدَّمَ، ثُمَّ صَلِّي} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

 

وَلِلْبُخَارِيِّ: {ثُمَّ تَوَضَّئِي لِكُلِّ صَلَاةٍ}

 

وَأَشَارَ مُسْلِمٌ إِلَى أَنَّهُ حَذَفَهَا عَمْدًا

 

Kutokwa kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: Faatwimah bint Abiy Hubaysh alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akauliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwanamke nakuwa na istihaadhwah (damu[5] ya haikatiki hata baada ya muda wa hedhi kumalizika) hivyo huwa sitohariki, je, niache kuswali?” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hapana kwani huo ni mshipa wa damu, wala si hedhi, hivyo, ukiingia katika hedhi, sitisha kuswali, na hedhi ikiisha, osha damu huko iliko, kisha uswali.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na katika Riwaayah ya Al-Bukhaariy ameongezea: “Kisha tawadha kwa kila Swalaah[6].”

 

 

MADHII YANAHARIBU UDHU

وَعَنْ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {كُنْتُ رَجُلاً مَذَّاءً، فَأَمَرْتُ اَلْمِقْدَادَ بْنَ اَلْأَسْوَدِ أَنْ يَسْأَلَ اَلنَّبِيَّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏فَسَأَلَهُ فَقَالَ: "فِيهِ اَلْوُضُوءُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ

 

Kutoka kwa ‘Aliy bin Abuu Twaalib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilikuwa mtu wa kutokwa na madhiy (majimaji yatokayo katika dhakari), nikamuamrisha Miqdaad bin Al-Aswad[8] amuulize Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), akamuuliza.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Anapaswa atawadhe.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

[Na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]

 

 

 

KUJAMBA KUNAONDOA UDHU

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{إِذَا وَجَدَ أَحَدُكُمْ فِي بَطْنِهِ شَيْئًا، فَأَشْكَلَ عَلَيْهِ: أَخَرَجَ مِنْهُ شَيْءٌ، أَمْ لَا؟ فَلَا يَخْرُجَنَّ مِنْ اَلْمَسْجِدِ حَتَّى يَسْمَعَ صَوْتًا، أَوْ يَجِدَ رِيحًا} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ

 

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu akipata kinachomtia shaka katika tumbo lake kuwa anatokwa kitu au la, basi asitoke Msikitini hadi amesikia sauti yake au ahisi harufu[10] yake.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

 



Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-09-03

ZOEZI

Jaza maswali yote ama baadhi kisha bofya kitufe za kutuma majibu hapo chini.



1 : Yafuatayo yanaweza kuondoa udhu wako isipokuwa______





2 : Mwanamke ambaye damu haikatiki baada ya kumaliza hedhi anatakiwa afanye nini ______





3 : Ukitokwa na madhii unatakiwa ufanye nini _____





4 : Nini ufanye endapo huna uhakika kama umejamba au hujajamba? _______





5 : yafuatayo yanaondoa udhu isipokuwa ________







RELATED POSTS

picture

AINA ZA NAJISI NA TWAHARA KATIKA UISLAMU

Post hii inakwenda kukufundisha aina za najis. Pia utajifunza aina za twahara katika uislamu
picture

JE MANII NI TWAHARA AU NAJISI?

Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis
picture

FADHILA ZA UDHU YAANI FAIDA ZA UDHU

Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu
picture

TWAHARA NA UMUHIMU WAKE KATIKA UISLAMU

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake
picture

JINSI YA KUTWAHARISHA AINA MBALIMBALI ZA NAJISI

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.
picture

MAMBO YALIYO HARAMU KWA MWENYE HEDHI NA NIFASI

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi
picture

ZIJUWE NGUZO TANO ZA UISLAMU NA MAANA ZAKE KATIKA SHERIA YA UISLAMU

Hili ni somo letu la kwanza kwenye mtiririko huu wa darsa za fiqh. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya uislamu na nguzo zake.
picture

JINSI YA KUTAWADHA KAMA AALIVYOTAWADHA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume