Zoezi - 1



1. Elimu ni nini?



2. “Sema, Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?...” (39:9)
Ni kwasababu gani wanaojua hawawi sawa na wasiojuwa?



3. Unatoa maoni gani iwapo wanaojua na wasiojua wakawa sawa kiutendaji?



4. Toa maelezo yenye ushahidi wa Qur-an kuonyesha kuwa:



(a)Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa binaadamu na Mola wake.



(b)Kutafuta elimu ni amri ya kwanza kwa bin a adam u.



5. Onyesha kwa ushahidi wa Qur-an kuwa katika Uislamu mgawanyiko wa elimu katika “elimu ya dini” na “elimu ya dunia” haukubaliki.



6. “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.” (96:1) Kusoma kwa jina la Mola wako maana yake nini?



7. “.... Soma na Mola wako ni karimu sana. Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu mambo aliyokuwa hayajui”. (96:3-5)
Orodhesha njia tano anazozitumia Allah (SW) katika kuwasiliana na wanaadamu.



8. Elimu yenye manufaa kwa binaadamu ni ile .................................



9. Eleza sababu tatu zinazopelekea elimu kupewa nafasi ya kwanza katika Uislamu.
*******************************


Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w) Kama tunavyojifunza katika surat ‘Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s.w). Allah (s.w) huwasiliana na binadamu na kuwaelimisha kwa kutumia mojawapo ya njia zifuatazo zilizoainishwa katika aya ifuatayo: Na haikuwa kwa mtu kwamba Mwenyezi Mungu anasema naye ila kwa il-hamu (anayetiwa moyoni mwake) au kwa nyuma ya pazia au humtuma mjumbe (Malaika) naye humfunulia kiasi anachotaka kwa idhini yake (Allah), bila shaka yeye ndiye aliye juu mwenye hekima.” (42:51). Aya hii inatufahamisha kuwa binaadamu hupata habari kutoka kwa Allah (s.w) kwa njia tatu zifuatazo: (a)Il-hamu(Intution). (b)Nyu ma ya pazia. (c)Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa. Pia katika Qur-an tunafahamishwa njia mbili nyingine anazozitumia Allah (s.w) katika kumfikishia binaadamu ujumbe kutoka kwake: (d)Ndoto za kweli (ndoto za Mitume).