Zoezi - 1
1. Elimu ni nini?
2. “Sema, Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?...” (39:9)
Ni kwasababu gani wanaojua hawawi sawa na wasiojuwa?
3. Unatoa maoni gani iwapo wanaojua na wasiojua wakawa sawa kiutendaji?
4. Toa maelezo yenye ushahidi wa Qur-an kuonyesha kuwa:
(a)Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa binaadamu na Mola wake.
(b)Kutafuta elimu ni amri ya kwanza kwa bin a adam u.
5. Onyesha kwa ushahidi wa Qur-an kuwa katika Uislamu mgawanyiko wa elimu katika “elimu ya dini” na “elimu ya dunia” haukubaliki.
6. “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba.” (96:1) Kusoma kwa jina la Mola wako maana yake nini?
7. “.... Soma na Mola wako ni karimu sana. Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu. Amemfundisha mwanaadamu mambo aliyokuwa hayajui”. (96:3-5)
Orodhesha njia tano anazozitumia Allah (SW) katika kuwasiliana na wanaadamu.
8. Elimu yenye manufaa kwa binaadamu ni ile .................................
9. Eleza sababu tatu zinazopelekea elimu kupewa nafasi ya kwanza katika Uislamu.
*******************************