Unatafakari kwa muda, unawaza ule asali bila hata ya kuhitaji maji, ama ukatafute maji kwanza. Pia una wazo eidha uendelee kuala asali
ama uendelee na kutafuta siri ilojificha katika maisha yako, juu ya nini kimekutokea.
Wakati unakaribia kutowa maamuzi yako, kwa mbali unasikia sauti ya Jogoo.... "HUENDA AKAWA NI NYOKA UYO...... AMA KUNA WATU KARIBU??"
Ni mawazo yako kwani ulisikia hadithi ya nyoka anayeweka kama jogoo. Ni nyoka hatari sana anayegonga utosini. Sasa umepata wazo lingine...