unaamua kula mkate, unaangalia saa yako ni saa 3:3 6pm. unakula mkate wako na kujitahidi kumeza. unakata kipande cha kwanza, cha pili
na hatimaye unamaliza nusu ya mikate ile miwili. Unapata wazo ni kwa nini kunguru amekufa, ghafla mikono inakutetemeka baada ya
kugunduwa kuwa huenda ikawa kuna sumu kwenye mikate.
unaanza kuangalia vipakti vile na unanusa, LOO!!!! ni sumu ya panya, ghafla tumbo linakuuma pamoja na kiu kikali sana. macho yanakosa nguvu
na kiza kinene kinatawala. Mapovu meupe yanakutoka na hatimaye umepoteza maisha kwa kula sumu.