kitabu cha mashairi

By Sukari ya mashairi

KITABU CHA MASHAIRI

SUKARI YA MASHAIRI
NENO LA AWALI:
Ni kitabu kilicho andaliwa kwa lugha ya kiswahili katika lugha iliyo nyepesi zaidi na yenye ufundi wa kishairi. Kitabu hiki kinapatikana kwa free yaani buree kutoka kwetu. Kwa yeyote anayetaka kukichapisha kitabu hiki awasiliana nasi kwa haraka zaidi.

Mtunzi wa kitabu hiki ni nguli chipkizi wa fani hii anayefahamika kwa jina la HD-Hassan. Kitabu hiki ni katika kazi zilizoandaliwa na mtunzi wetu huyu wa mashairi. Tumetarajia katika kitabu hiki kuelimisha na kuburudisha na si vinginevyo. Kama na wewe ni mshairi chipkizi na unataka kazi zako ziweze kusambawa nasi. Wasikiana nasi kwa 0620555380 au 0655832944 WhatsApp.

SHAIRI: CHUKI
Kwako lifike darasa, lisilo lamembarini, Lisilo hitajipesa, adakama yashuleni, Litambue hili kosa, silitie matendoni, Mvaach u ki moyoni, mwenyewe h uja mtesa, Kisikie hikikisa, utafakari kichwani, Sichakale nicha sasa, sikiliza kwamakini, Upate kiini hasa, nakipi utabaini, Mvaa chuki moyoni, mwenyewe huja mtesa, Bwana mmoja afisa, wacheo serikalini, Alie akitikisa, kwa mbwembwe zote mjini, Mkewe ekuwa tasa, ndio wake mtihani, Mvaa chuki moyoni, mwenyewe huja mtesa, Nduguye damu kabisa, kwake hali masikini, Ekuwa na wana tisa, na wakumi e tumboni, Ikatokea furusa, kuitwa kibaruani, Mvaachuki moyoni, mwenyewe huja mtesa, Bwana akaanza visa, vya kuvunja tumaini, Ila ndugu hakususa, akatazama usoni, Kumbe kilichomtesa!, apate vyote kwanini? Mvaa chuki moyoni, mwenyewe huja mtesa, Lilo likimtonesa, atarithiwa nanani, Nahakutaka kabisa, wale wana wafulani, Donda hilo halebesa, lemuweka taabani, Mvaa chuki moyoni, huja mtesa mwenyewe, Kufumbua na kupwesa, aondolewa cheoni, Bila kosa bila kisa, karudi uriyani, Machungu akaalisa, kwahuzuni na nun'guni, Mvaa chuki moyoni, hujamtesa mwenyewe, Shida kuanza mnusa, msaada hauoni, Hana nduru hana hisa, akangia majutoni, maisha yakibubusa, ikawa kwake ngani, Mvaa chuki moyoni, mwenyewe huja mtesa,

KUTOA NI USHUJAA
Salamu kwanza awali, wasikizi tikieni, Mwambaje nazenu hali, kheri nawatakieni, Mungu awape sahali, muifuzu mitihani, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Kila alie akili, hutunza yake thamani, Hilo sote twakubali, sitaraji upinzani, Zingata yangu kauli, ikufae maishani, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Mja ulie na mali, mtazame masikini, Kwani wake udhalili, niqadari ya manani, Kumtenga niajali, tena mbaya hukumuni, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Natena usikubali, aingie dhilalani, Maliyo siibakhili, nikuipa kisirani, Mungu kwayake ajili, mlinde huyojirani, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Kumwacha niukatili, tena usio kifani, Fikiria mara mbili, mali kwakomtihani, Hakutatosha kuswali, namisaada toweni, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Ukitaka afadhali, nauishi kwa amani, Mafunzo haya nakili, uyatie matendoni, Kiombwa siwe mkali, toa kwadhati moyoni, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Maisha nipande mbili, kuna nyuma na usoni, Ukatae ukubali, lambeleni hulioni, Kesho hashindwi jalali, nawe kukushusha chini, Kutoa niushujaa, ubakhili nitamaa, Mtu nzi:H D.Hassa n @SUKARI YA [email protected] Pangani Tanaga 0655832944

NDEGE WAFIKISHE
Hebu paa ndege paa, ufise habari hizi, Ufike wanako kaa, imi kufika siwezi, Paa bila kuzubaa, upae anga iwazi Naujumbe huu twaa, tekeleza hiikazi, Kawa pe utawafaa, wata po fa nyia kazi Kwa watakaokataa, usifanye lazimizi, Wambie lamanufaa, niwasihilo mtunzi, Elimu iso chakaa, ni ifanyiwayo kazi, Ili wawe mashujaa, waepuke upuuzi, Waache kata tamaa, katikalao amuzi Subira ikiwajaa, lilofichwa huja wazi, Shidani wakikomaa, lazima lije tatuzi, Wasivunje ujamaa, sababu yamachukizi, Wasiishi kwahadaa, nichukizo kwa mwenyezi, Nawaache kuzubaa, wafanyapo andalizi, Wambie elimu taa, kuikosa niajizi, Mwenye elimu hun'gaa, sioleo tangu juzi, Ujinga kizaazaa, mfano kama uchizi, Yasaba beti nakaa, sitaki uendelezi, Shikeni hayo kadhaa, yalainishe ulezi, Tungo hii nibidhaa, nawaipe mapokezi, Mtu nzi:H D.Hassa n Tanga pangani 0655832944


Pata kitabu Chetu Bofya hapa